MSHAMBULIAJI wa zamani wa Manchester United, Louis Saha, amesema kuwa haikuwa sawa kumlinganisha chipukizi Alejandro Garnacho na supastaa wa Al-Nassr Cristiano Ronaldo.

Garnacho mwenye umri wa miaka 18 ameibuka kuwa mmoja wa vipaji vilivyokua Old Trafford tangu ajiunge nayo kutoka Atletico Madrid kwa £420,000 mwaka 2020.

Amecheza mechi kadhaa akiwa na Mashetani Wekundu chini ya Erik ten Hag na ameonyesha uwezo wake uwanjani kwa uchezaji wake wa umeme kwenye mbawa.

Saha aliulizwa kwenye Betfred kuhusu Garnacho kufananishwa na Ronaldo mchanga. Akimsifu winga huyo, alijibu:

“Naona machoni pake [Garnacho] kwamba anataka kucheza, hata hivyo huwezi kumlinganisha mtu yeyote na Cristiano Ronaldo Hakuna kulinganisha kabisa.

“Cristiano ni simba na hana dharau kwa Garnacho, lakini kama anaweza kuwa nusu ya Cristiano ni sawa kabisa.”

Leave A Reply


Exit mobile version