Wakati wengine wakiendelea kuupitia mkeka wa leo kutoka Kijiweni ni wazi kwamba wapo ambao hubashiri kwa kiasi kikubwa katika zile mechi moja moja na miongoni mwa mechi hizo ni kama hii ya Brentford dhidi ya Man City mchezo wa ligi kuu ya Uingereza utakaopigwa katika dimba la Gtech Community.

TAKWIMU

Katika michezo yao 7 ya mwisho ya ligi kuu ya Uingereza kabla ya kukutana na Man City hii leo, klabu ya Brentford wamepoteza michezo 6 huku wakishikilia nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza. Alama 3 pekee zinazowatofautisha na wanaotaka kushuka daraja.

Man City wao katika michezo yao 8 ya mashindano yote wameshinda michezo yote hivyo kuwa tishio sana kwa Brentford japokua wako nyumbani.

  • Brentford wanataka kuweka rekodi ya kuifunga Man City mara 3 mfululizo
  • Pep Guardiola hajawahi kupoteza mechi 3 mfululizo kiushindani hapo kabla ya kukutana na Brentford ambao wameshinda michezo 2.
  • Man City katika michezo 2 kati ya 4 na timu za ligi kuu ya Uingereza kutoka London ameruhusu bao.
  • Brentford hawajawahi kupata sare katika michezo yao 8 ya mwisho katika uwanja wao wa Gtech ambapo wameshinda 4 na kufungwa michezo 4
  • City ameshinda michezo yake 3 ya mwisho ya ugenini ligi kuu ya Uingereza.

 

TUNABETIJE?

Wakati Brentford wao wakitaka kusaka rekodi mbele ya City na kujiweka sawa katika msimamo wa ligi upande wa pili nao wako tayari kuhakikisha kuwa nao wanashinda ili kukaa sawa katika msimamo wa ligi mbele ya Arsenal na vinara Liverpool.

  1. Man City anashinda
  2. Magoli zaidi ya 2 yaani Total Goals Over 2.5
  3. Kutakua na kufungana yaani Both Team to score – YES

 

SOMA ZAIDI: Nini maana ya Anytime Goalscorer katika betting?

Leave A Reply


Exit mobile version