Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema anataka “timu bora” kushinda taji la Premier League msimu huu.

Klopp alikuwa akizungumza baada ya Wekundu hao kutoka sare ya 2-2 na Arsenal siku ya Jumapili.

The Gunners walikimbilia kuongoza kwa mabao mawili ndani ya nusu saa ya kwanza, shukrani kwa Gabriel Martinelli na Gabriel Jesus.

Hata hivyo, Mohamed Salah alirudisha bao moja kabla ya mapumziko. Huku Roberto Firmino akisawazisha mchezo ikiwa imesalia dakika moja.

Matokeo hayo yanawafanya Arsenal wabaki pointi sita mbele ya Manchester City, lakini mabingwa hao wamecheza mechi moja pungufu.

Klopp alifuatwa na AFTV alipokuwa akiondoka Anfield na kuulizwa ni nani angependa kushinda taji hilo.

“Nataka timu bora kushinda,” alijibu kwa urahisi.

Leave A Reply


Exit mobile version