Wakati Brentford wakiishangaza United na kikosi cha Erik ten Hag mnamo mwezi Agosti, wakipata ushindi wa 4-0, lakini hakukuwa na dalili ya kurudia ushindi huo usiku uliokuwa huko Manchester, huku rekodi ya Manchester United ya kushindwa kufunga ikivunjwa kwa ustadi na Rashford.

Staa huyo, ambaye alicheza kama mshambuliaji wa kati baada ya kukoseakana Wout Weghorst, aliunganisha mpira uliopigwa na Marcel Sabitzer kwa kichwa dakika ya 27, akifunga kwa ustadi na kuipa United alama tatu muhimu huku wakirudi kwenye mbio za kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.

Rashford sasa amefunga mabao 10 ya ushindi katika ligi msimu huu, sawa na Wayne Rooney mwaka wa 2009-10.

Brentford walionekana kuwa na msisimko mdogo sana baada ya kutoa sare mechi ya 3-3 na Brighton siku nne kabla, mechi ambayo walikuwa wakiongoza kwa bao 3. Kuchoka kulianza kuonekana kwenye kikosi cha Thomas Frank, ambacho hakikua na madhara na kufanikiwa kupiga shuti moja tu lililolenga lango.

“Sio kiwango chetu cha juu kabisa,” kocha Frank alikiri baada ya mechi, huku kocha wa upande wa pili Ten Hag akizungumzia kurejesha viwango baada ya kushindwa 2-0 dhidi ya Newcastle siku ya Jumapili.

“Mtu yeyote anajua kwamba hatuwezi kucheza vizuri kila wiki, lakini hakuna wakati wa kupunguza viwango vyetu na tunapaswa kuendelea kujaribu kusukuma kila mmoja,” Marcus Rashford aliongeza.

Leave A Reply


Exit mobile version