IlipoishiaNdiyo! Unapaswa kukubali kuolewa na Osman ili apone na  afanyiwe upasuaji wa kupandikiza figo” Mama alirudia kauli  yake, akili yangu ilihama na kumuwaza Mosses, maneno  aliyoyasema wakati naondoka kwake, achilia mapenzi yangu  kwake 

“Mama naweza vipi kuolewa na Osman, siyo chaguo langu lile,  wala siyo aina ya Mwanaume ninayemtaka katika Maisha yangu,  Mama nina Mtu wangu….Siwezi” Nilisema huku nikiwa ninalia,  chozi lilikuwa likinivuja. Endelea 

SEHEMU YA TISA

Aliingia Bilionea Dhabi, alitukuta tukiwa katikati ya  maongezi yetu. Mzee Dhabi aliponiona alitabasamu tuu, alikuwa  ameongozana na Mke wake ambaye ni Mama Mzazi wa Osman,  Alinisogelea kisha aliniambia 

“Jacklin! Hujakosea, upo sahihi, ni ngumu sana kuolewa na  Mwanaume ambaye hayupo ndani ya moyo wako, upo sahihi sababu  huwezi ndiyo maana uliondoka jana Usiku. Lakini Jacklin, hebu  tazama macho ya Mama yake Osman, ona lile chozi kwanza”  Niligeuza macho yangu kumtazama Mama yake Osman, Ni kweli  alikuwa akivuja mchozi 

“Analia kwasababu Osman ni Mtoto wake wa kipekee, hana Mtoto  mwingine kama ulivyo wewe kwa Mama yako, lile chozi ndilo  ambalo Mama yako alikuwa akilia wakati alipopoteza tumaini la  wewe kuishi. Unakumbuka kilichotokea, Mungu alimleta Osman  katika Maisha yako, alipambana hata kutoa figo lake ili  upone, hakufanya kwa ajili ya mapenzi bali kwa huruma yake  kwa Mama yako, ulilala Jacklin hukumuona Mama yako alivyokuwa  anahangaika hata kutaka kutoa figo lake akuwekee wewe”  Bilionea Dhabi alizungumza maneno mazito sana ambayo  yalimfanya Mama ajiinamie akiwa analia 

“Nakuomba sana Jacklin, okoa Maisha ya Mwanangu, hatuna Mtoto  mwingine zaidi yake, Osman ndiye Maisha yetu, kufa au kupona  kwa Osman kunakutegemea wewe Jacklin” Alisema Mzee Dhabi  kisha alienda kuketi kando ya Mke wake, maneno yake  yalinifanya nishindwe kuendelea kuketi pale sebleni  nilikimbilia chumbani kwangu. Ni kweli Osman alijitoa na  kuhakikisha Maisha yangu yanarudi, tumaini la Mama yangu  linarudi, leo yupo Kitndani na Mimi ndiye ninayepaswa  kumuamsha, Daaah roho iliniuma sana. 

“Usilie Mama Jacklin, Binti yako ni Mtu mzima anajuwa  anachokifanya. Kama amekataa kumsaidia Osman hakuna njia  nyingine tutaondoka naye kuelekea Dubai tukajaribu huko,  ikishindikana basi haikuwa ridhki yetu kuwa na Osman” Alisema  Baba yake Osman, Mama yake Osman alikuwa akilia huku akiwa  amejifunika na kitambaa alishindwa hata kusema chochote, Mama  yangu alinyanyuka na kunifuata chumbani, alinikuta nikiwa  nimeshikilia simu yangu, alisogea kisha aliketi kando yangu  kwa upole sana alisema 

“Jacklin Mwanangu! Nilikuzaa na kukulea katika Mazingira ya  kujuwa nini Maana ya utu na shida, pengine ndiyo nguvu  iliyomvuta Osman kuja kwenye Maisha yako, alikuja kama Masia  akaokoa Maisha yako, leo amegeuka kikwazo cha furaha yako.  Nikiwa kama Mama yako nakueleza jinsi ninavyojisikia Jacklin”  Alisema Mama kisha alifikicha jicho lake moja ambalo lilikuwa  likimwaga chozi

“Moyo wangu umevunjika Jacklin, furaha imenitoweka kama  Kizimikavyo kibatari wakati wa upepo Mkali, Jacklin Mama yako  nimeumia sana. Siku Osman akiondoka hapa Duniani ndiyo  itakuwa mwisho wako kusikia sauti yangu, yule Kijana  alirudisha tumaini kwenye moyo wangu, alinifanya nijisikie  amani sana lakini leo umeiondoa yote” Mama alisema,  nilitamani kumjibu na Kumwambia kuwa kama nitaolewa na Osman  basi Mosses atasambaza video zangu za faragha, hadi Mama  anaondoka chumbani kwangu mdomo wangu ulikuwa mzito sana kama  samaki aliyejaza maji mengi 

Niliangalia ujumbe ambao Mosses aliutuma, alikuwa  akinikumbusha kuwa endapo nitamuacha atasambaza hizo video,  nilivujisha chozi machoni mwangu. Yalikuwa ni maumivu makali  sana ambayo hata sikuwahi kuyahisi katika Maisha yangu.  Nilipaswa kuokoa Maisha ya Osman kama ambavyo aliokoa yangu  ila ningefanya kitu gani? Kama video zitasambaa naweza hata  kujitoa uhai kukwepa aibu nzito lakini je Mama yangu Mzazi  akiziona video hizo naye atakuwa katika hali gani? Vipi  Familia ya Osman itajisikia vipi, ndio maana nasema kilikuwa  ni kipindi kizito na kigumu kwangu. 

Mama aliporudi Sebleni hakuwakuta Baba na Mama yake Osman,  aliangusha kilio kama kuna Mtu amefariki, nilishtuka na  niliumia sana. Nyumba ilikosa ile amani iliyokuwepo Mwanzo,  ukimya ulitawala hakuna aliyetoa neno lolote zaidi ya sauti  za kufungwa na kufunguliwa kwa milango. Nilijitupa kitandani  nikawaza sana nifanye jambo gani ili kumsaida Osman bila  kuchukua uamuzi ambao ungesababisha kusambaa kwa video hizo  za faragha. Kadili nilivyokuwa natulia kitandani ndivyo picha  ya tukio la kukataa kuvishwa pete na Osman lilivyokuwa  linajirudia katika akili yangu, nilikosa utulivu kama Mtu  anayesumbuliwa na mizimu, niliamka bado Mama alikuwa  akiendelea kulia, nikiwa kama Mtoto nilijivuta kwenda  kumbembeleza. 

Nilimkuta akiwa amekaa chini ameegemea sofa, niliketi kwa  adabu na utulivu mkubwa sana, Mama alihisi ujio wangu  alitulia kimya huku akihema sana. Nilishusha pumzi zangu  kisha nilisema 

“Samahani Mama najuwa nimekuvunja moyo ila..” Kabla hata  sijamaliza nilichokitaka kukisema Mama alinikatisha 

“Ishia hapo hapo Jacklin, Wazazi ambao Mtoto wao aliokoa uhai  wako wameondoka kwasababu umekataa kuokoa uhai wa Mtoto wao,  nimeonekana Mama mbaya sana, Mama mbinafsi ambaye hajali  kuhusu Mtoto wa mwingine” Alisema Mama kisha aliendelea

“Kama Osman atakufa basi juwa ni kwasababu yako, hupaswi  kusameheka katika hilo Jacklin” Alimaliza kusema kisha  alinyanyuka na kwenda zake chumbani kwake, chozi  lilinimwagika Mimi Jacklin niliona kila Kiti kipo dhidi  yangu, sikuwa na Mtu wa kunisemea kabisa. 

Usiku ulipofika niliondoka nyumbani nilienda kulala Hotelini,  nilihitaji muda wa kuwa peke yangu ili niweze kutafakari  mambo kwa umakini zaidi. Nilizima simu zangu ili nisipate  usumbufu wowote ule, hakuna aliyejuwa niko wapi, Si Mosses  wala Mama yangu niliyemwambia, nilitaka kutafakari ili nijuwe  nafanya nini katika kipindi kigumu kama hiki. 

Hali ya Osman haikuwa nzuri kabisa kule Hospitalini, alikuwa  kila azindukapo anataja jina langu tu, alikuwa anachomwa  sindano za usingizi ili kumtuliza. Familia ya Bilionea Dhabi  iliingia gizani, tumaini lao juu yangu liliondoka kabisa,  wakiwa nyumbani kwao Mke wa Bilionea Dhabi alimwambia Mume  wake 

“Twende kwa mara ya mwisho kuzungumza na Jacklin kama  atakataa kwa kinywa chake basi hatutokuwa na namna nyingine  bali kuondoka na Osman” Alisema kwa sauti ya Kimama iliyojaa  maumivu ya kumuona Mtoto wake akiwa kitandani na hana tumaini  lolote lile 

“Sasa hata kama tutafanya hivyo Mama Osman, Binti hawezi  badili msimamo wake, hampendi Osman na hilo lipo wazi sana”  Alijibu Baba yake Osman, Mara mlango uligongwa 

“Ingia” Alisema Bilionea Dhabi baada ya kumtambua aliyekuwa  akigonga, alikuwa ni Mlinzi 

“Samahani Baba na Mama, kuna mgeni hapo nje anasema anahitaji  kuonana na Osman” Alisema Mlinzi huyo baada ya kuwa tayari  ameingia ndani, Mzee Dhabi aliangalia saa yake aliona ni  mishale ya saa 4 za Usiku alimuuliza Mlinzi 

“Huyo Mtu yupoje?” 

“Mwanamke, mweupe” Alisema Mlinzi kisha alitabasamu tu baada  ya alichotaka kukisema kuhisi hakina maana hapo mbele ya Mzee  Dhabi na Mke wake lakini Mzee Dhabi alimuelewa Mlinzi  akamrahisishia 

“Mzuri Eeh” Basi mlinzi alitoa tabasamu zito 

“Mh! Atakuwa Nani huyo!” Alisema Bilionea Dhabi kisha  alitafakari

“Utamjuwa vipi bila kumuona, Mlete” Alidakia Mke wa Mzee  Dhabi. Mara moja Mlinzi aliondoka, dakika moja baadaye  alirudi akiwa ameambatana na Mgeni huyo 

Mzee Dhabi na Mke wake walisimama kwa Mshangao Mkubwa sana  baada ya kumuona Mgeni huyo kisha Mzee Dhabi alisema 

“Mlinzi nenda” Mlinzi aliondoka zake 

  • ••••••••••••••••••••••••••• 

“Zahra?” 

“Zahra?” Mzee Dhabi na Mke wake alisema kwa pamoja baada ya  kumuona Zahra mbele yao, Si unamkumbuka Zahra? Ni yule  Mwanamke aliyechota kiasi kikubwa cha pesa na kutimkia zake  Ughaibuni, alikuwa ni mpenzi wa Osman ambaye aliuteka moyo wa  Osman miezi kadhaa iliyopita aliondoka na kusema kuwa ana  Mwanaume mwingine hivyo Osman asihangaike kumtafuta, tukio  hilo lilisababisha Osman kupata Mshituko na kukimbizwa  Hospitalini. 

Zahra alishtuka kuwaona Wazazi wa Osman, alitetemeka kwa Hofu 

“Hebu keti” Alisema Mzee Dhabi, wote waliketi kisha Mzee  Dhabi na Mke wake walitazamana 

“Ni wewe Zahra au tunaota ndoto ya Mchana?” Aliuliza Mama  yake Osman 

“Ni Mimi Mama naomba msamaha wenu kwa kila kilichotokea,  natamani kumuomba msamaha Osman na ndiyo sababu ya kuja hapa”  Alisema Zahra 

“Unataka kumuomba Msamaha Osman?” 

“Ndiyo Baba! Najuta kwa kila nilichomfanyia. 

“Nifuate” Alisema Mzee Dhabi, walitoka ndani Bilionea Dhabi  na Zahra, waliingia kwenye gari ya kifahari ya Mzee huyo  kisha safari ilianza, Zahra hakujuwa alikuwa akipelekwa wapi 

“Baba tunaenda wapi?” Alihoji Zahra 

“Si umesema unataka kumuomba msamaha Osman? ” 

“Ndiyo Baba” 

“Tunaenda alipo Osman”

Usiku huo nilikuwa nimeamua jambo moja, kumsaidia Osman  kwasababu alisaidia Maisha yangu, akili yangu iliniambia kuwa  Osman alikuwa mwenye huruma na mapenzi ya kweli kuliko Mosses  ambaye alianza kutishia kusambaza video zangu za Faragha.  Niliondoka Hotelini nikaelekea nyumbani, Nilipochungulia  ndani nilimuona Mama akiwa amekaa kando ya Mlango wa  kuingilia ndani nilijuwa tu alikuwa akinitafuta japo  alinichunia, nilitabasamu sababu Mama yangu alikuwa ni Mama  mwenye upendo wa Hali ya juu sana kwangu, nilifuangua geti,  nilitupa macho upande wa kushoto nililiona lile gari  aliloninunulia Osman kwenye siku yangu ya Kuzaliwa, moyo  uliniuma sana. 

Nilisogea alipo Mama kisha nilimwambia 

“Mama nipeleke Hospitalini alipo Osman” Kauli yangu ilimfanya  Mama anitazame mara mbili mbili 

“Mama moyo wangu unaniambia tufanye haraka sana” Nilisema  nikiwa kwenye hali ya Haraka, lilikuwa ni jambo ambalo Mama  alikuwa akilisubiria. Haraka alikimbilia ndani akatoka na  mtandio, tulitoka tukachukua Tax kisha safari ya kuelekea  Hospitali ilianza. 

Upande wa pili, Baba Osman na Zahra walikuwa wanaingia  Hospitalini, walisogeza gari kwenye maegesho kisha walielekea  Wodini ambako Osman alikuwepo 

“Baba Osman anaumwa? Mbona umenileta Hospitalini?” Aliuliza  Zahra 

“Ndiyo Osman ni Mgonjwa sana ndiyo maana nimekuleta hapa  Zahra” Alijibu Baba Osman, walishuka kisha walielekea ilipo  wodi hiyo. Bahati nzuri walikutana na Dokta Simon ambaye  alikuwa akitoka wodini humo, alipomuona Zahra alishangaa sana 

“Najuwa una maswali mengi Simon lakini hiyo ndiyo hali  halisi” alielezea Mzee Dhabi baada ya kuisoma sura ya Dokta  Simon ilivyokuwa 

“Lakini Mzee, Osman hapaswi kushtushwa na jambo lingine  mnaweza kumpoteza kabisa, kwanini aje leo?” 

“Maswali yako Simon hayawezi kujibiwa kwasasa, nina imani na  hiki atakachokiona Osman” Aliesema Mzee Dhabi 

“Lakini sikushauri kabisa kwenda huko Mzee Kwasasa yupo Macho  angalau anajisikia vizuri mgesubiria kidogo basi” alisema  Dokta Simon

“Mimi ni Baba yake Osman, najuwa nini nafanya Simon….Twende  Binti” Alisema Mzee Dhabi akiwa amemshika mkono Zahra,  waliingia wodini bila kusikiliza alichokisema Dokta Simon 

Kitendo cha kufungua mlango kilihamisha macho ya Osman,  aligeuza na kuangalia aliposikia sauti ya Mlango kufunguliwa.  Alitoa macho yake, alijaza hewa kwenye kifua baada ya kumuona  Zahra Mwanamke ambaye alimfanya ayachukie Mapenzi, Mwanmke  ambaye alimtafuta sana Ughaibuni bila Mafanikio. 

Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya KUMI Ya PUMZI YA MWISHO

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM  

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

SOMA KISASI CHANGU HAPA  

SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

 

Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx 

  

9 Comments

  1. Dah naona kesho mbal tuendeleee hadith imejoga sasa apo kwa akili ya haraka haraka julieth akimuona zarha atagoma ten kumhudumia osman 🤞🤞🤞uwiiiiiiiiiiii hadith tam nyie 💔💔💔💔💔💔🤕🤕🤕🤕🤕NATAFTA MPENZ KAMA OSMAN🤕

  2. Mshtuko umuue osman wazazi wa osman wamfukuze jack moses amuache jack mama yake ammchukie hyo pumzi itakuwa ya mwsho

Leave A Reply


Exit mobile version