IlipoishiaYote yaliyo mema, mazuri na yenye uelekeo mzuri zaidi, muda  siyo mrefu maono yangu yatadhihirika” Sikutaka kuendelea  kumuuliza, nilimwambia 

“Sawa Mama nasubiria hayo Mema, nipo chumbani kwangu”  Nilisema kisha nilielekea Chumbani kwangu, tulikuwa tukiishi  Watu watatu tu, yaani Mimi, Mama na Mdada wa kazi. Hadi  naondoka sikujuwa Mama na Osman walikuwa wamewasiliana na  kuambiana kuwa nilienda kwa Osman. Endelea 

SEHEMU YA SABA

Ila ndani ya moyo wangu nilihisi amani sababu tayari nilikuwa  nimeshamuomba msamaha Osman, na pia nilikuwa nimeweka mambo  sawa kwa Mama yangu. Siku zilipita, niliendelea na kazi,  Mapenzi yangu kwa Mosses yaliendelea bila tatizo lolote tena  alikuwa akininyenyekea sana tofauti na mwanzo, kazi  ziliendelea kule kwenye kampuni ya Osman, niliendelea kupata  uzoefu huku ukaribu kati yangu na Osman ukizidi kuongezeka.  Osman alikuwa akiumwa sana ila alikuwa akijikaza mno mbele  yangu ila sura yake ilionesha wazi kuwa alikuwa akiumwa,  sikutaka kumuuliza sana sababu kama ningekuwa na unuhimu wa  kulijuwa hilo angelikuwa ameshaniambia muda mrefu.

Alinipeleka sehemu mbalimbali, ndani na nje ya Nchi,  alinifundisha vingi sana Osman. Namna tulivyokuwa tumezoeana  kama ikitokea umetuona kwa mara ya kwanza ingekuwa rahisi  kuhisi ni wapenzi, Osman alikuwa akijaribu kunionesha hisia  zake lakini hakusema kwa kinywa chake, nakumbuka siku yangu  ya kuzaliwa alininunulia gari aina ya Cadilac, aliniandalia  kila kitu kwa ajili ya siku yangu ya kuzaliwa, nilimuarika  Mosses kwasababu ndiye Mwanaume aliyekuwa akinipa furaha. 

Mama aliniita pembeni, akaniuliza 

“Hivi Jacklin unatumia ubongo wako vizuri kuwaza?” Aliuliza  kwa sauti ya Juu sababu kulikuwa na kelele za Mziki, wakati  huo Watu ndio walikuwa wakifika nyumbani kwetu kwenye hiyo  sherehe ya siku ya kuzaliwa 

“Mama! Nimefanya kitu gani kibaya?” Nilimuuliza 

“Mosses amefuata nini hapa? Hii ni sherehe yako wewe, Osman  amefanya kila kitu bado unashindwa hata kumuheshimu?” Alisema  Mama ilinibidi nishushe mzuka wangu 

“Hivi Mama kwanini tunaishi kwa kuhofia fulani atasema nini?  Osman ni rafiki yangu, na Bosi wangu. Kuniandalia sherehe  haimaanishi mimi na yeye ni wapenzi Mama, Nitasherehekea vipi  siku yangu ya kuzaliwa bila Mosses?” Nilimuuliza Mama 

“Huyo Mosses anajulikana na nani? Amekusaidia nini hadi hivi  sasa kama siyo kula pesa yako ambayo imetokana na Osman?  Jacklin, hujui kilichopo kichwani kwa Osman na hujui kwanini  aliandaa hii sherehe yako ya kuzaliwa. Unaiyona ile gari  pale? Ile ni zawadi kutoka kwa Osman, huyo Mosses wako  anaweza kukununulia japo Pikipiki?” Mama alisema na niliona  wazi alikuwa amepaniki. 

“Samahani Mama” Nilisema, nilikuwa sipendi kumuona Mama yangu  akiwa katika hali ya kuhuzunika kisa Mimi 

“Mwambie huyo Mosses aondoke hapa kabla Osman hajafika, Osman  ni mfadhili wetu hivyo ni lazima tuheshimu hisia zake” Mama  alisema Maneno ya mwisho kisha aliondoka pale, aliniacha na  mawazo lukuki sana nikajiuliza maswali mengi ambayo sikuwa na  majibu yake 

Nikiwa nimesimama alikuja Mosses akiwa ameshikilia glasi  yenye kinywaji, aliniuliza 

“Mama alikuwa anasemaje? Nimewaona kama mlikuwa mkigombana  hivi” nilimtazama Mosses kisha nilitabasamu tu nikamwambia

“Hapana kuna jambo alikuwa ananielekeza ndio tukawa  hatuelewani, lakini usijali” nilisema 

“Mlisema Sherehe inaanza saa moja usiku, sasa inakimbilia saa  mbili, anasubiriwa nani?” Aliuliza Mosses, nilikosa cha  kumjibu. Mara zilisikika honi za gari huko nje, 

“Wageni hao hebu twende” Nilisema lakini Mosses alinishika  mkono akanivuta pembezoni kwenye mnazi. Alitupa glasi  pembeni, akaanza kunila mate yangu. Nilishindwa kujizuia  nikajikuta namba sapoti Mosses, eneo ambalo sisi tulikuwa  tumesimama lilikuwa na mwanga hafifu sana. 

Wakati magari yanaingia sisi tulikuwa bize kupeana mate pale  kwenye mnazi, bahati mbaya Osman aliangalia tulipo japo  hakunitambua kutokana na lile giza. Alikuwa ameingia na Baba  na Mama yake, Zilipokuja kuwashwa taa zote ndipo tuliposhtuka  tukaacha ule mchezo, ila mashine ya Mosses ilikuwa imesimama.  Tuligawana njia, mimi nilipitia upande wangu na Mosses upande  wake, nilipowaona Wazazi wa Osman nilishangaa sana sababu wao  walikuwa Dubai au inamaana walikuja kwa ajili ya Sherehe  yangu ya siku ya kuzaliwa tu au kulikuwa na jambo  lililowaleta pale? Nilisimama kwa sekunde kadhaa kabla ya  kujitokeza huku bado mawazo yakiwa yananizonga kichwani  kwangu, sikuamini Sherehe yangu ya kuzaliwa ihudhuriwe na  Bilionea Mkubwa kama Baba yake Osman? 

Nilipojitokeza sikuonesha dalili yoyote kuwa nilikuwa  nimetingwa na mawazo, nilienda kumsalimia Baba yake Osman,  alikuwa akinipenda sana na mara zote alikuwa akisema natembea  na kiungo chao japo alikuwa akisema kama utani ila ilikuwa ni  kweli nilikuwa natembea na figo ya Osman, tulicheka pamoja,  nilipogeuka nilikutana na Mama yake Osman naye alitabasamu,  tulisalimiana vizuri sana, ilikuwa ni sherehe ndogo  iliyobadilika na kuwa kubwa tena yenye heshima sana hadi Watu  tuliowaarika walishangaa. Walinionesha mahali alipo Osman,  alikuwa amesimama na rafiki zake, nilienda kumsalimia huku  macho yangu yakimtafuta Mosses alipo, Osman alinikumbatia  kisha alinishika mkono huku akiendelea kuniuliza maswali ya  hapa na pale 

Punde shughuli ilianza, Mama yangu sikumuona kabisa licha ya  kupepesa macho huku na kule. MC wa shughuli aliniita katikati  ya Watu waliokuwa wamesimama, nilitembea taratibu sababu  nilivalia gauni refu lenye rangi ya Dhahabu. Nijisifie tu  maana ukisubiria kusifiwa hapa Duniani utazeeka, nilipendeza  mno.

“Leo ni siku nzuri na nyenye baraka kutoka kwa Mungu, ndugu  yetu Jacklin leo ametimiza miaka 28. Bahati ilioje kwake ni  kwamba sherehe yake imehudhuriwa na Bilionea ambaye ndiye  Baba wa Osman ambaye pia ameandaa shughuli hii kwa ajili ya  Jacklin” Alisema MC kisha Watu walipiga makofi mengi sana,  bado nilikuwa nikiangaza macho yangu kumtafuta Mosses, bahati  nzuri nilimuona akiwa amesimama nyuma akiwa anaangalia tukio  lilivyokuwa likiendelea. 

Nilitabasamu ili tu mambo yaende ila nilipoteza uwezo wa  kujiamini kabisa, MC aliendelea 

“Namkaribisha Osman Dhabi aje mbele atuambie siku ya leo  amemuandalia nini Jacklin” Makofi mengi yalipigwa, Bilionea  Mzee Dhabi naye alikuwa akifurahi pamoja na Mke wake hapo  ndipo nilipomuona Mama yangu akiwa amesimama kando ya familia  hiyo ya Kitajiri, Mama alinipa ishara ya kukubali  kitakachotokea pale, nilishindwa kumuelewa ni kwanini  nikubali kwasababu sikujuwa kilichotaka kwenda kutokea. Osman  alipofika karibu na Mimi alisema 

“Wakati nakutana na Jacklin kwa mara ya kwanza nilimuona ni  Mwanamke Msumbufu, asiyejali, mkorofi lakini nilivyokuja  kumuelewa niligundua ni Mwanamke wa tofauti sana” Alisema  Osman, wote walipiga makofi hata Mimi nilitabasamu maana  nilikumbuka jinsi nilivyokutana na Osman kuanzia kwenye  Pikipiki hadi kwenye mvua, nilicheka. 

“Kwa muda mfupi anenitengenezea kumbukumbu zisizofutika  katika Maisha yangu, leo kwenye siku yake ya kuzaliwa  nilifikiria ni zawadi gani naweza kumpa ili afurahi, niliona  nimnunulie gari aina ya Cadilac escaled ya Mwaka 2021”  Shangwe ziliibuka pale, makofi yalipigwa sana 

“Gari hii ina thamani ya Milioni 600, ni zawadi ambayo moyo  wangu umeridhia kwake lakini pia napenda kumuomba Jacklin”  Alisema Osman kisha alipiga magoti akanitazama, nikaiyona  ishara kuwa anataka kunivika pete kidoleni, nilishtuka  nilipomuona Akitoa pete kwenye mfuko wa koti lake la suti 

“Nipe ruhusa niwe Mumeo Jacklin, maneno haya si rahisi Mtoto  akayazungumza mbele ya Wazazi wake lakini nimeshindwa  kufikisha hisia hizi kwako, nimeona leo ni wakati sahihi wa  kufanya hivi” Nilimtazama Osman kama vile nataka kumuuliza  maswali ambayo hata sikujuwa niulizaje, nilipogeuza macho  nilikutana na Mosses, Mama na Wazazi wa Osman, wote walikuwa  kimya kusikiliza nitasemaje. Niliishiwa nguvu jamani

Osman alinishika mkono akawa ananivisha ile pete taratibu,  nilikuwa kama Mgonjwa wa koma, ghafla nilishtuka nikasema 

“Hapana Osman, siwezi” nilisema kisha niliivua ile pete  nikamtupia Osman, Watu walijawa na mshangao mkubwa sana,  Chozi lilimbubujika Osman 

“Jacklin tafadhali, fanya kwa ajili ya Wazazi wangu nakuomba”  Alisema Osman 

“Siwezi Osman, siwezi kuidhurumu nafsi yangu, siwezi kuuza  upendo wangu Osman, unajuwa fika nina Mtu wangu” Nilisema,  Watu walikuwa kimya sana kusikiliza maongezi yetu 

“Jacklin, hili ni ombi langu kwako, baada ya hapa sitakuwa na  uwezo wa kukuomba chochote tena, tafadhali” Alisema Osman  kisha aliushika mkono wangu ili anivishe tena ile pete,  nilimsukuma kisha niliondoka pale, nilikimbilia nje kabisa,  Mosses alinifuata huko nje, tulichukua Bajaji na kuondoka  pale nyumbani. Nilipomsukuma Osman alianguka, hali yake  ilibadilika alikimbizwa Hospitalini, Hekaheka ilikuwa kubwa  pale nyumbani, Watu walikuwa wakijiuliza kulikoni, Mzee Dhabi  alihangaika kwa ajili ya Mtoto wake. Muda mchache watu  waliondoka pale nyumbani, alibakia Mama akiwa analia tu, nami  nilikuwa nikilia ndani ya Bajaji, siyo kwamba nilikuwa  simpendi Osman ila tayari nilikuwa na Mwanaume niliyempenda  ambaye ni Mosses. 

Nilikuwa nimeshabadilisha hali ya hewa, nililia sana nikiwa  ndani ya Bajaji, Mosses alinibembeleza hadi tulipofika kwake. 

Tukiwa chumbani aliniuliza 

“Nini kinaendelea Jacklin?” Aliniuliza akiwa amekaa pembeni,  chozi lilikuwa likinibubujika, nilimuwaza Mama yangu,  nilijuwa nimemkosea sana. 

“Mosses, hakuna chochote kinachoendelea kati yangu na Osman,  nimeshangaa ameita wazazi wake kwenye sherehe yangu ya  kuzaliwa istoshe hakuwahi kuongelea kuhusu mapenzi  nimeshangaa alipotaka kunivesha pete” Nilisema huku nikiwa  najifuta mchozi, simu yangu ilikuwa ikiita sana na aliyekuwa  akinipigia alikuwa ni Mama yangu, niliamuwa kuizima kabisa. 

“Yule ndiyo amebadilisha Maisha yenu?” Aliniuliza “Ndiyo Mosses, ni yeye”

“Haiingii akilini Mtu aje tu atake kukuvesha pete, lazima  kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea kati yenu” 

“Mosses tafadhali naomba uniamini, nisingelimkimbia kwa ajili  yako, ile ni familia ya kitajiri sana. Kama siyo wewe  ningelikuwa nimekubali lile jambo ila upo wewe Mwanaume  nikupendaye Mosses” nilisema kisha nilimuona Mosses  akitafakari jambo, kilio changu kilikata nikawaza labda  alikuwa anataka aniache 

“Hebu tuliza akili yako Jacklin, kesho asubuhi tutaongea  jambo moja” Alisema Mosses, nilipata muda wa kupumzika. 

•••••••• 

Mama yangu hakulala, hakula chakula, alikesha kunipigia simu  bila kupokea majibu yoyote. Usiku ulikuwa mwingi ilimbidi  aingie ndani, Usiku huo taarifa kutoka maabara zilisema hali  ya Osman inaweza kuwa mbaya zaidi baada ya miezi mwili  kutokana na figo lingine kufanya kazi kwa kiwango kidogo  sana. Taarifa hii ilikuwa mbaya na isiyopendeza kabisa, Mzee  Dhabi na Mke wake walihuzunika sana, walimuuliza Dokta Simon 

“Kwanini hukusema kabla Osman hajachukua uamuzi wa kuondoa  figo moja?” Ilikuwa ni sauti yenye maumivu sana iliyotoka  kwenye kinywa cha Bilionea Dhabi 

“Niliongea naye kabla ya kuchukua uamuzi huo, cha ajabu  alimuhamisha mgonjwa na kwenda kufanya upasuaji India,  aliniomba nisiwaambie chochote kwasababu alikuwa na uhakika  wa kupata figo haraka iwezekanavyo. Tukio lililotokea leo  siyo tu limemletea mshituko bali mfadhahiko mkubwa ndani  yake” Alisema Dokta Simon, Chozi lilimbubujika Mama yake  Osman, alikuwa ndiyo Mtoto wao wa pekee hawakubatika kupata  Mtoto mwingine 

“Laiti kama mioyo ingekuwa inahamishika basi ningehamisha  moyo wa Osman, mara zote tuliamini tukimpa pesa nyingi Mtoto  wetu itampa jeuri na kuondoa mapenzi katika Moyo wake lakini  Osman amekuwa dhahifu sana linapokuja suala la Mapenzi” Mzee  Dhabi alimtuliza Mke wake 

“Dokta inahitajika huduma gani kwa Mtoto wangu, Hospitali  gani Duniani, Pesa Kiasi gani? Nipo tayari kutoa nusu ya  utajiri wangu kwa ajili ya Osman” Alisema Mzee Dhabi, Dokta  Simon alimwambia Mzee Dhabi 

“Unaweza ukapata figo, ukapata kila kitu lakini huwezi  kuuondoa mfadhahiko alionao Mwanao. Kitu cha kwanza ni kumuondolea mfadhahiko Osman ili kumuandaa kwa ajili ya  upasuaji wa kupandikiza figo” Alisema Dokta Simon 

“Pesa siyo tatizo Simon, niambie hiyo huduma inapatikana  Hospitali gani Duniani, kiasi gani kinahitajika?” Aliuliza  Bilionea Dhabi, walionesha kumpenda sana Mtoto wao. 

“Mfadhahiko huondolewa na kilichosababisha mfadhahiko,  tumaini alilokuwa nalo ndilo lenye kuuondoa huo mfadhahiko wa  Osman” 

“Unamaanisha nini?” 

Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NANE Ya PUMZI YA MWISHO

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM  

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

SOMA KISASI CHANGU HAPA  

SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

 

Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx 

5 Comments

Leave A Reply


Exit mobile version