August 3 Mwaka 2018 Young Africans iliachana na jumla ya wachezaji 14 kisha wakabaki na majina ya wachezaji wasiozidi 17 ndani ya kikosi chao ambao, katika orodha ile ya wachezaji walioachwa kulikuwa na majina kama David Molinga, Mrisho Ngasa, Jaffary Mohamed, Tariq Seif, Andrew Vicent, Papy Kabamba Tshishimbi na Mohamed Issa ambao mikataba yao ilimalizika na hawakuongezewa

Kipindi hiko Young Africans ilisitisha mikataba yao ni Raphel Daud, Yikpe Gislain, Ali Ali, Patrick Sibomana, Muharami Issa, Ally Mtoni Sonso(Marehemu) na Eric Kabamba! Hapo katika idadi ile ya wachezaji 17 waliobaki ni wanne tu ndio walikuwa Raia wa Kigeni ambao ni Haruma Niyonzima, Farouk Shikalo, Lamine Moro na Bernard Morrison

Baada ya hapo Timu ilicheza misimu mitatu(2018/19, 2019/20 na 2020/21) bila Ubingwa wa Ligi Kuu, walikubali kufanya mabadiliko na hata hiyo Miaka mitatu bila Ubingwa bado waliishi kwenye nafasi mbaya na walifanya mabadiliko ya wachezaji wengi sana ndani ya kikosi

Walicheza ‘Four Seasons’ bila Ubingwa wa Ligi Kuu na waliamua kufanya kitu cha tofauti baada ya kufeli! Kwanza kurudisha mashabiki karibu na Timu yao, kufanya uchaguzi wa Viongozi ambao wana maono ya kupeleka chapa ya klabu yao mbali zaidi na kufanya Usajili wa wachezaji Bora tofauti na walioondoka! Timu ikarudi kwenye mstari mpaka sasa inafanya vizuri

Simply! Mantiki yangu ni kwamba kwa sasa SIMBA SC wanatakiwa kufanya maamuzi ya haraka hasa ndani ya uwanja, Timu inahitaji kubadili eneo kubwa sana la wachezaji waliopo ambao tayari wameipa Timu nyakati zao bora! Simba inahitaji ‘Quality Players’ wengi ambao wataiaogeza chapa ya MNYAMAA zaidi ya hapo ilipo

Kwakuwa eneo kubwa la wachezaji inaonekana linatakiwa kupungua pale basi wakati ndio huu! Wachezaji wengi ambao wameingia ndani ya Klabu wamefeli kati ya 100%, naona wamefeli 70% na wamefaulu 30% wamefaulu

Simba SC iwapo watafeli tena kwenye eneo la Usajili basi hizi nyakati zitaendelea kuishi kwao, Abdelhack Benchikha anahitaji sura mpya ili kurudisha ubora wa Timu na kusukuma ‘Vision & Mission’ ya Klabu hasa kwenye CAF Tournaments! That is Truth about LUNYASI

SOMA ZAIDI: Waraka Mzito Wa Hamisi Kigwangalla Kuhusu “Kuinunua Simba”

15 Comments

  1. Ukweli unauma🍃 Kwasababu haiwezekani Team inacheza michezo yote na bado wachezaji wote hawajafikia mabao ya mchezaji alieondoka..hiyo ni kumaanisha kuna upungufu mkubwa wa Quality Players

  2. Yes mnyama apunguzee zaidi wazee katika timu ili vijana wapate nafasi kunawatu umri umeendaa inabidi wawache vijanaa na kuongeza sula mpya Runyasi👍👍👍👊🏻

  3. Kidullahson HL on

    Upo sahihi 👊🏻
    Ila mimi kwa mtazamo wangu, viongozi ndio wenye wajibu wa kuleta quality players, wanaofeli sio kwamba hawajitumi ila uwezo wao ndio umeishia hapo, kuna usemi unasema ‘you cannot offer what you don’t have’ so Mangungu na viongozi wenzake Wakatakiwa kuwajibika kwa kuwa kwa misimu yote mitatu wameleta wachezaji wasioendana Na vision za club yq simba sc. Kama hawawezi kuleta wachezaji wanaoweza kuendanq na Maono ya club that’s absurd na wanatakiwa kuwajibika haswaaa 😞😞

  4. Ukweli ni kwamba …

    Kama wachezaji ni wa low quality na hawawezi kubeba maono ya club imekuaje wakasajiliwa na kuwa part ya club…??
    Kwa tasfiri nyingine na kwa harak harak tu itabidi ufikilie ni wakinanani waliohusika na mchakato mzima huo adi club yetu pendwa kufikia apo ……
    Hapo ndipo itabidi tushughulike na mizizi ya tatzo ilo kabla ya kuchukia matunda yke ndipo tutakapo geukia kwa viongozi na kamati yao kuhusu wachezaji ni swala la mwisho baada ya kushughulikia utendaji wa viongozi ..

  5. Kwangu Mimi sioni kama wachezaji ndio wanashida🤔 shida Iko kwenye management nzima ya Simba na UKISIKIA kitu management inaanzia juu kuja chini kwahyo huwezi kulahumu wachezaji kuwa ndio wanafelisha timu ya Simba hapana management ndio Ina wajibu wakukaa na kujua tatzo ni Nini ukilahumu wachezaji kwani hawaingii wa uwanjani na je wakiingia hawachezi….mfano mechi ya Yanga Africans na Simba juzi wachezaji walifanya vizuri sana lakini shida ni kwamba management ya Simba inashindwa kuhafikiana hili ikaleta mabadiliko ndani ya timu na kuludi katika mstari

  6. Mh, mnadhani hii timu mbona imefanya vzuri hadi sasa,, kwani iko nafasi ya ngapi? Au kwakuwa imefungwa na Yanga nje ndani?

    Utafika wakati wao he he he

  7. Uongoz wa simba ndo tatizo umesajil wachezaj wa ajabu na wamafungu ,,yanga kipind kile haikua na hela je simba ya sasa haina hela

  8. Pingback: Uchambuzi Wa Mechi JKT Tanzania vs Yanga Lawama Uwanja? - Kijiweni

  9. Pingback: Mchezaji Gani Wa Nje Hapa Ligi Kuu Amekuwa Bora Zaidi Kwako? - Kijiweni

Leave A Reply


Exit mobile version