Ilipoishia 

“Ingia kwenye gari” ilikuwa kama ndoto vile, nilifungua  mlango wa gari ili niingie kwenye gari. Kabla hata sijaingia  nilihisi uzito kwenye mgongo wangu alafu nilipata nguvu ya  kuuliza 

“Nani wewe!” Niliuliza kwa sauti ya juu mno kisha niliona  kama vile Dunia ilikuwa imesimama, ghafla nilisikia sauti ya  kugongwa kwa mlango. Mara nilijikuta nikirushwa pembeni,  nilitumia nguvu ya mwisho kuangalia niliona pikipiki  ikianguka kando yangu ndipo nilipogundua kuwa nilikuwa  nimepata ajali ya Pikipiki. Sikuelewa kilichoendelea, mzimu  wa laana na matatizo uliendelea kuniandana. Endelea 

SEHEMU YA SABA

Nilizinduka nikiwa Amana Hospital, daktari alikuwa kando  yangu akiangalia jinsi nilivyokuwa nikiamka kutoka katika  Usingizi mzito wa ile ajali, nilikuwa na maumivu makali ya  Mgongo 

“Tulia utakuwa sawa” Alisema Daktari huyo ambaye alianza  kukagua macho yangu kisha aliniuliza 

“Unaitwa Nani?” 

“Naitwa Jojo” nilijibu kwa maumivu makali sana. 

“Unaishi wapi?” Aliniuliza, nilitikisa kichwa ishara ya kuwa  nilikuwa sina makazi 

“Ndugu zako wapo wapi?” 

“Sina ndugu hapa, wapo Tabora…..aliyenileta hapa yupo  wapi?” Nilimuulizia yule Msanii 

“Umeletwa hapa na wasamalia wema tu hata hivyo wameondoka  zao” 

“Msanii hajafika hapa?” 

“Hakuna aliyekuja kukuona” Alijibu yule Daktari kisha  aliniambia 

“Unapaswa kwenda soba kwanza ili kukuondoa kwenye matumizi ya  madawa, vipimo vimeonesha damu yako inakiwango kikubwa cha  madawa ya kulevya” Alisema yule Daktari kisha alisema 

“Gharama zote zitalipwa na Hospitali” 

“Asante sana” nilisema, nilifurahi kwa upande mmoja sababu  sikupenda kuwa Mtumwa wa madawa ya kulevya tena. 

Nilipopata unafuu nilipelekewa Soba, nilifundishwa vitu vingi  mno, nilikutana na wengine ambao walikuwa wameathirika zaidi  na Madawa ya kulevya, niliishi huko kwa zaidi ya miezi sita  hadi nilipopona kabisa na kuacha matumizi ya dawa za kulevya.  Baada ya hapo, nilikabidhiwa kwa Mama mmoja ambaye alikuwa  akiitwa Mama Zahara, alikuwa ni Mama fulani mnene hivi 

“Utaenda kuishi kwake sababu huna mahali pa kwenda kuishi,  huko mtaani utarudi tena kwenye ulevi” Alisema Mtu wa Soba.  Nilifurahia sana kwenda kuishi kwa huyo Mama, niliona naenda  kufungua ukurasa mpya wa Maisha yangu, ukurasa ambao  utatengeneza upya Maisha yangu.

“Utaishi kwangu kwa Muda kisha utaamuwa kama utaendelea au  utarudi kwenu Tabora” Alisema Mama Zahara, basi tuliingia  kwenye gari yake kisha tulienda nyumbani kwake, alikuwa na  nyumba nzuri sana kubwa ambayo alikuwa akiishi na Wasichana  waliotoka Soba. 

Niliishi hapo kama Mwanafamilia, Maisha yalikuwa mazuri sana,  tulipewa kila kitu, hadithi za walio wengi pale walikuwa  hawana makazi kama Mimi, wengine waliondoka na wengine  tulibakia. 

Miezi miwili ilikatika nikiwa hapo kwa Mama Zahara, Siku moja  Mama Zahara alisafiri, alituaga kuwa anaenda Mombasa Kenya.  Alituhasa sana kuendelea kuishi kwa upendo wa hali ya juu  sana na pia kuishi kwa kujali afya na malengo yetu,  alipoondoka kila mmoja aliachiwa pesa yake kwa ajili ya  kujikimu kidogo maana alikuwa anaenda kukaa huko kwa kipindi  cha mwezi mmoja. 

Kulikuwa na Mdada aliyeiywa Salome, tulijenga ukaribu sana,  alikuwa na hela nyingi kuliko Msichana yeyote pale, nilipata  shahuku ya kumuuliza 

“Hivi Salome hizo pesa unatoa wapi?” Kwanza alicheka kisha  alinijibu 

“Nazitafuta Jojo, unafikiria pesa inaokotwa?” 

“Sijamaanisha kuwa inaokotwa ila nimeuliza ili nijuwe” 

“Jibu zuri ni matendo, kesho ni Jumamosi, usiku tutoke”  Alisema Salome, alikuwa ni Mdada fulani mnene kiasi mweusi,  macho yake yalikuwa makubwa 

“Usiku tena?” 

“Ndiyo, hofu yako ndiyo umasikini wako, ni lazima Jojo  ujifunze kutengeneza pesa kwa ajili ya Maisha yako,  unafikiria siku ukiondoka hapa kwa Mama Zahara utapewa pesa  ya kuanzia Maisha? Utapewa nauli tu, sasa utaishi vipi huko  kwenu?” Alisema Salome, maneno yake yalikuwa na mashiko  kwenye ufahamu wangu, alichokisema niliona kina ukweli 

“Sawa tutaenda” Nilimkubalia bila kujuwa alikuwa anataka  kunipeleka wapi, wakati huo ule uzuri wangu ulikuwa umerejea  tena kwa kasi sana sababu nilikuwa naishi vizuri sana pale  kwa Mama Zahara.

Siku iliyofuata Usiku tulitoka tukiwa tumevalia vinguo  vifupi, japo nilimuuliza tulikuwa tunaenda wapi ila  aliniambia nitaona, nilimuamini sababu alikuwa ndiye rafiki  yangu pale kwa Mama Zahara. 

Tulichukua Taxi hadi Magomeni, ilikuwa mishale ya usiku wa  saa tano, tulipofika aliniambia tusubirie. Tulisimama  barabarani tu, baridi lilikuwa kali sana pale kiasi nilikuwa  najikunyata. 

“Tutasimama hadi saa ngapi Salome? Mimi nimechoka” nilisema,  kiukweli tulisimama kwa zaidi ya nusu saa, alikuwa  akisimamisha magari binafsi ya Watu lakini yalikuwa  hayasimami 

“Salome nimechoka mwenzio” Nilisema huku hasira ikianza  kunishika 

“Unataka kuharibu sasa si ndiyo?” 

“Salome hii ni Biashara ya Ngono unaifanya si ndiyo? Sasa si  bora ungeniambia kule nyumbani unafikiri ningekuja huku Mimi?  Yaani sijui mimi nakuwaje Aisee huwa naingizwa kwenye mambo  yasiyofaa kirahisi sana” Nilisema kwa kujilaumu, Salome  alirudi kuendelea kusimamisha gari 

Nilikaa pembeni, Idadi ya Wanawake hapo ilianza kuongezeka,  walivalia kama sisi tulivyovaa na wengine walikuwa wakivuta  sigara, niliyachukia Maisha yale kabisa, nilimfuata tena  Salome 

“Kama huwezi kuondoka na Mimi basi nitaondoka mwenyewe  Salome” Nilisema 

“Nipe dakika tano tu nakuomba Jojo kisha tutaondoka” Alisema  Salome 

“Sawa ni dakika tano tu baada ya hapo sitakuwa na muda wa  kuendelea kukusubiria” Nilisema kisha nilirudi kuketi kando  kidogo ya waliposimama wao 

Baadaye niliona gari ikisimama, Salome alianza kuzungumza na  Mtu wa kwenye gari japo sikusikia walichokiwa anakizungumza  ila nilihisi itakuwa amepata Mteja 

Alikuja akaniambia 

“Si ulikuwa unataka kwenda nyumbani? Basi wewe nenda mimi  nitarudi asubuhi” Alisema Salome

“Sasa ulichoniletea huku ni nini Salome? Aaah” nilisema kwa  kuchukia sana 

“Nenda Jojo tutaongea nyumbani ila usimwambie Mtu yeyote”  Alisema Salome kisha alikimbilia kwenye gari akapanda kisha  gari iliondoka. Nilichukia mno istoshe kiatu kilikuwa  kinanibana sana mguu wa kushoto, niliamuwa kukivua ili  nisizidi kuumia. 

Nilisimama pembezoni mwa waliposimama wale wanawake  wanaojiuza, nilikuwa nasubiria gari ya kurudi nyumbani.  Ghafla nilisikia purukushani, nilipogeuka niliona wale  wanawake wakikimbia huku na kule huku wakipiga mayowe.  Nilihamaki, nilihitaji kujuwa wamepatwa na nini, punde  niliona Watu waliovalia sare za polisi. 

Nami nilianza kukimbia, polisi wawili wakawa wananikimbiza,  walinikamata mita chache tu kabla hata sijafika mbali. 

“Naomba mniache tafadhali” nilisema wakiwa wananipeleka  kwenye gari ya polisi 

“Wanawake wa Siku hizi bwana, Mwanamke mzuri kama wewe  ujiingize kwenye biashara ya ukahaba, twende tukakufundishe  kazi huku” Alisema Askari mmoja 

“Mimi siyo kahaba nilikuwa nasubiria gari nirudi nyumbani,  sijawahi kuuza mwili katika Maisha yangu” Nilijaribu  kujitetea kidogo ili niachwe. 

“Twende utajuwa huko huko kama ulikuwa ukiifanya hiyo  biashara au ulikuwa hauifanyi” Alinijibu yule askari 

“Kweli mimi sijafanya kama mnataka nimpigie ndugu yangu  ambaye nilikuja naye huku” Nilisema tena 

“Ndugu yako atakuja kituoni kutoa maelezo huu siyo muda wa  maelezo” Alinijibu Polisi mwingine, tayari tulikuwa  tumeshafika kwenye gari. Waliniingiza kwenye gari ya Polisi,  Wale makahaba nao walikuwa wamekamatwa pia. 

Tulipelekwa kituo cha Polisi, tulitupwa Mahabusu. Siku  iliyofuata niliitwa na Polisi nikaambiwa niwapigie ndugu  zangu ila kibaya sikuwa na simu wala namba ya Mtu kichwani,  angalau ningempigia Salome au hata Mama Zahra lakini hata  hivyo Mama Zahra alikuwa nje ya Nchi ningempata vipi? 

“Afande siijui namba ya Ndugu yangu hata mmoja ila naomba  nipo chini ya Miguu yako twende nyumbani kwetu, 

watakuthibitishia kuwa Mimi sijiuzi kabisa” Nilisema, yule  Polisi alicheka akasema 

“Hayo ndiyo maneno yenu, nakusikitikia sana Ndugu yangu  sababu Rais ametoa maagizo makali sana kuhusu Biashara  mnayofanya, siku tatu zijazo mtafikishwa mahakamani na  mtahukumiwa kufungwa Miaka mitatu au Faini isiyopungua  Milioni 6” Alisema yule Polisi 

“Kaka yangu wewe una ndugu au hata Dada kama Mimi, naomba  usimame kama Kaka kwangu niangalie Mdogo wako ninavyoteseka”  Nilisema 

“Nikisema nisimame kama Kaka nitasimama kwa wangapi?  Tutakomesha hii Biashara kweli? Nenda ukafunzwe na Walimwengu  huko uendako” Alisema kisha nilirudishwa Mahabusu. Ni Mimi  peke yangu ndiye niliyekuwa nikilia ndani ya Mahabusu sababu  sikuzoea maisha yale kabisa. 

Nilionekana kero kwa wale mahabusu wengine wakawa wananisema  sana nijikaze sababu Biashara ile ndiyo kila kitu, nilijaribu  kuwaambia kuwa Mimi siyo kahaba ila hawakutaka kunielewa  kabisa wakasema kama siyo kahaba nilifikaje pale? Na  nilijuana vipi na Salome wakati Salome ni kahaba wa muda  mrefu? 

Sikuwa na utetezi kabisa, niliishia kulia tu. Ukurasa wangu  mzuri wa Maisha ambao ulifunguka na kunipa furaha sana  ulianza kuchanika, nilijikuta nikirudi kwenye Maisha  yaliyojaa giza tena, niliishi hapo kwa hizo siku mbili na  hakuna aliyekuja kunitafuta. 

Siku ya tatu tulipelekwa Mahakamani, Polisi walisimama kama  Mashahidi, nililia sana Mahakamani ili niachiwe lakini  haikusaidia. Hakuna hata mmoja kati yetu aliyekuwa na kiasi  cha Shilingi Milioni 6 ili asifungwe, sote tulihukumiwa  kifungo cha miaka mitatu. 

Tulipelekwa gerezani, siku tunavalishwa sare za Gerezani na  kukatwa nywele zetu ndipo nilipoamini kuwa nilikuwa  nimetumbukia kwenye shimo lenye giza, nilifikiria Miaka  mitatu ilivyokuwa Mingi nitaweza kuishi gerezani kweli? Kama  kulia nililia sana hadi mwili ulishika moto lakini hakuna  kilichosaidia, kilio changu na machozi yangu yaligeuka kuwa  chozi la samaki lisombwalo na maji, hakuna aliyenisikia wala  kuthamini chozi langu, kila Mtu alikuwa na matatizo yake  ndani ya Gereza hivyo isingelikuwa rahisi kusikilizwa.

Nilikubaliana na hali halisi, niliyaanza Maisha mapya ndani  ya gereza. Maisha yaliyojaa ubabe, uonevu, utata, manyanyaso  na kazi ngumu sana. Tulifanya kazi ngumu na kupewa chakula  kidogo tena hicho kidogo anakuja Mtu anakuchukulia kwa ubabe  wake na hakuna cha kumfanya. 

Nilimpata rafiki ndani ya gereza, aliyeitwa Isabela naye  alikuwa Mtu wa Tabora hivyo tulikuwa na memgi ya kuzungumza.  Yeye alihukumiwa kwa kosa la kumkata Mkono kimada wa Mume  wake, japo tulikuwa katika nyakati ngumu sana ila tuliishia  kucheka tuu maana hakukuwa na njia nyingine zaidi kutumikia  adhabu, Mume wake hakuwahi kuja kumuangalia Gerezani kwa  miezi zaidi ya mitatu. Isabela alihukumiwa kifungo cha miaka  miwili tu 

“Ukishamaliza kifungo una mpango gani?” Nilimuuliza Isabela  tukiwa shambani tunalima 

“Kurudi Tabora tu maana nimegundua Mume wangu hanipendi  kabisa licha ya kumzalia Mtoto mmoja, angekuja kuniona  angalau ningekuwa na tumaini. Ila najutia sana hasira zangu,  ona nateseka mwenyewe kwa ajili ya mtu ambaye hajali chochote  kuhusu Mimi” Alisema, niliona jinsi alivyokuwa na maumivu  moyoni, ghafla nilijiona sina matatizo kabisa. 

“Pole sana Isabela, yataisha tu. Ukifika Tabora nenda  nilipokuelekeza waambie nipo Gerezani” Nilisema. 

Basi Maisha ndani ya Gereza yaliendelea, siku moja baada ya  kazi ilikuwa ni majira ya saa 7 Mchana, ulikuwa ni muda wa  kupata Chakula. Tulikuwa tukipanga mistari miwili kwa ajili  ya kupata Chakula, msitari wa kwanza nilikuwepo Mimi, sasa  katika tazama tazama nilistaajabu nilimuona Sarafina, yule  Mdada ambaye alifukuzwa na Shonaa kisa Mimi, nilitamani  kumuita ila nilikumbuka kuwa alikuwa na hasira na Mimi,  nilimgeukia Isabela nikamuuliza 

“Yule yupo hapa kwa muda gani?” Nilimuonesha kidole Sarafina 

“Nimemkuta hapa, anaonekana kahukumiwa muda mrefu ila  inasemekana aliiba pesa kwa tajiri mmoja” 

“Vipi unamjuwa?” 

“Ndio namjuwa” Basi baada ya kuwa tumeshachukua chakula  tulienda kula, Isabela aliniuliza 

“Unamjua vipi yule” 

Nini Kitaendeea?  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST? 

Usikose SEHEMU YA NANE ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM  

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

SOMA KISASI CHANGU HAPA  

SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

 

 Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx  Mungu Amenisahau xx 

 

  

6 Comments

Leave A Reply


Exit mobile version