Mkurugenzi Mtendaji wa klabu hiyo, Richard Arnold, anatarajiwa kuondoka Old Trafford kabla ya mwisho wa mwaka huu huku klabu hiyo ikijiandaa kwa uwekezaji wa Sir Jim Ratcliffe.

Arnold alitwaa nafasi ya Ed Woodward kama Mkurugenzi Mtendaji wa United miaka 21 iliyopita, lakini inaonekana kwamba Sir Jim Ratcliffe hana nafasi ya kumpa ndani ya Old Trafford.

Kulingana na ripoti ya Sky, Arnold ataondoka kabla ya kampuni ya Ineos Group ya Ratcliffe kuthibitisha ununuzi wao wa asilimia 25 ya hisa katika klabu.

Arnold ameshikilia nyadhifa kadhaa ndani ya United tangu mwaka 2007, na uongozi wake mfupi kama Mkurugenzi Mtendaji umefanana na kipindi cha Erik ten Hag kama meneja.

Hii imesababisha kushambuliwa kwa jinsi United walivyofanya shughuli zao wakati wa dirisha la uhamisho msimu huu, ambao umefuatiliwa na mwanzo mbaya zaidi wa msimu katika kipindi cha miaka 60.

Msimu huu pekee, United wameleta wachezaji kama Rasmus Hoijlund, Mason Mount, Sofyan Amrabat, Andre Onana, Jonny Evans, Sergio Reguilon, na Altay Bayindir, ambapo wachezaji wengi wao wamekosolewa kwa nyakati tofauti katika msimu ambao umekuwa na changamoto nyingi hadi sasa.

Kulingana na Mark Kleinman wa Sky Sports, Mshauri Mkuu wa kisheria wa United, Patrick Stewart, atachukua nafasi ya muda kama Mkurugenzi Mtendaji mara tu Arnold atakapoondoka.

Stewart ataendelea kutekeleza majukumu yake ya sasa na bado haijulikani ni nani atakayeingizwa kama mrithi wa muda mrefu wa nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji.

United bado hawajathibitisha rasmi uwekezaji wa Sir Jim Ratcliffe katika klabu, lakini wanatarajiwa kutangaza jambo hilo wiki ijayo.

Baada ya kutumia miaka 16 ya kazi yake katika United, haieleweki Arnold ataelekea wapi baadaye.

Kuhusu umiliki wa klabu kwa ujumla, licha ya maandamano na hasira ya mashabiki dhidi ya Glazers, Waamerka hao wanatarajiwa kuendelea kubaki madarakani, hata baada ya uamuzi wa Ratcliffe wa kuwekeza.

Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa

Leave A Reply


Exit mobile version