Ni KMC ambao wamefanikiwa kubaki Ligi Kuu msimu ujao kwa kuwafunga Mbeya City kipigo cha mabao 2-0 ikiwa ni mchezo wa marudiano uliofanyika katika uwanja wa Uhuru.

Mabao yote yalipatikana katika kipindi cha kwanza bao lilofungua dimba likipatikana dakika ya tatu lililofungwa na Daruweshi Saliboko na kumaliziwa dakika 27 na Aweso Aweso.

KMC walipishana kwa alama moja katika msimamo wa Ligi huku watoto wa Kinondoni wakiwa na pointi 32 na Mbeya City kuwa na pointi 31.

Mbeya City imebakiza nafasi moja ya lala salama watakapokutana na Mashujaa  kucheza play off itakayoamua safari yao ya kubaki Ligi Kuu msimu ujao.

Mchezo huo wa muhimu kwa pande zote mbili utafanyika tarehe 19 katika uwanja wa Lake Tanganyika na marudiano yatamalizika tarehe 24 June uwanja wa Sokoine Mbeya.

Huku Mashujaa wanapigania kupanda Ligi Kuu na Mbeya City wakitamani kusalia kundini.

Kwa taarifa zaidi za michezo tufuatilie hapa.

Leave A Reply


Exit mobile version