Inter Milan wamepata pigo kubwa katika harakati zao za kumsajili kipa Anatoliy Trubin wa Shakhtar Donetsk, ambaye amechagua kujiunga na Benfica kama kituo chake kijacho.

Fabrizio Romano anaripoti kuwa Benfica wamemaliza mkataba na mlinda lango huyo wa Ukraine, wakikubali kulipa kiasi cha euro milioni 10 pamoja na euro milioni 1 kama nyongeza.

Nerazzurri walimtaka Trubin kwa muda mrefu wakati wa majira haya ya kiangazi kama mrithi wa muda mrefu wa Andre Onana, ambaye alisaini mkataba na Manchester United.

Lakini mazungumzo na klabu ya Ukraine yalikuwa magumu kwa vigogo wa Italia, ingawa Trubin alitaka kuhamia Inter Milan.

Inter pia walikuwa na mpango mbadala wa kumsajili kijana huyo mwenye umri wa miaka 22 bila malipo wakati mkataba wake utakapomalizika msimu ujao, lakini mpango huo pia umefutwa.

Hata hivyo, Nerazzurri wako karibu kumsaini mlinda lango wa Bayern Munich, ambaye kwa sasa yupo Milan kwa vipimo vyake vya afya.

 

Inter wamefikia makubaliano na Bayern Munich baada ya mazungumzo magumu kuhusu mlinda lango huyo raia wa Uswisi, ambaye atahamia San Siro kwa mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya euro milioni 6.

 

Inasemekana Sommer amekamilisha sehemu ya kwanza ya vipimo vyake vya afya leo na anatarajiwa kusaini mkataba wake hivi karibuni.

Mwenye umri wa miaka 34 atakuwa chaguo la kwanza langoni, huku Simone Inzaghi akikusudia kusajili makipa wawili zaidi endapo Samir Handanovic na Alex Cordaz watatoka.

Baada ya kukosa kumsajili Trubin, Inter sasa wamelenga kipa Emil Audero wa Sampdoria na kipa mchanga Bento wa Athletico Paranaense.

Kwa upande mwingine, Nerazzurri wanatarajiwa kutangaza usajili wa kiungo wa Serbia Lazar Samardzic baada ya kufikia makubaliano na Udinese.

Folarin Balogun wa Arsenal anashikilia nafasi ya juu kwenye orodha ya washambuliaji wa Inter baada ya kukosa kumsajili Romelu Lukaku na Gianluca Scamacca.

Baada ya kupata pigo la kukosa kumsajili kipa waliyemtaka kwa muda mrefu, Inter Milan sasa wameelekeza nguvu zao kumtaka kiungo wa kati Lazar Samardzic kutoka Udinese.

Usajili huu unatarajiwa kuongeza nguvu katika safu yao ya kati na kuboresha uwezo wao wa kusukuma mbele mashambulizi.

Soma zaidi: habari zetu kama hizi hapa 

Leave A Reply


Exit mobile version