Meneja wa zamani wa Tottenham Hotspur, Harry Redknapp amedokeza kwamba mshambuliaji Harry Kane angependelea kujiunga na mahasimu wa klabu hiyo Chelsea badala ya Manchester United.

Kane amekuwa akihusishwa na kuhamia Manchester United na Chelsea msimu huu wa joto.

Nahodha huyo wa Uingereza anaingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Tottenham Hotspur.

Hata hivyo, Redknapp anaamini kuwa itakuwa hatua nzuri kwa Kane kujiunga na Chelsea kwani anajenga nyumba katika eneo hilo na hasa ikiwa Mauricio Pochettino, ambaye alikuza maendeleo yake huko Spurs, atateuliwa kuwa mrithi wa kudumu wa Graham Potter huko Stamford Bridge.

“Itakuwa ya kuvutia kama Pochettino ataenda Chelsea,” Redknapp aliambia Beyond the Pitch podcast.

“Hilo halitawaendea vyema mashabiki wa Tottenham hata kidogo, hilo ni la uhakika. Ni hatua nzuri kwake na nadhani yeye [Harry Kane] anajenga nyumba katika eneo hilo.

“Yeye ni mtu wa familia na angefurahi zaidi kutohamia kaskazini mwa Uingereza au popote atakapolazimika kwenda.”

Leave A Reply


Exit mobile version