Ilipoishia “

Baada ya kumaliza maongezi walirudi sebuleni, Gorii” alitembezwa nyumba nzima ajue mazingira pia alipatiwa chumba chake kwaaajili ya mapumnziko.

Mwisho kabisa walikaa mezani wapate chakula Cha pamoja. Mama Doreen aliomba kuondoka huku akimwahidi Gorii atamletea nguo zake. “

Endelea

SEHEMU YA TANO

Ilipita Kama wiki mbili Gorii” tayari alikuwa amezoea mazingira, tangu akae pale hakuona dalili yoyote ya kutengwa zaidi familia ya Mzee Mishoki ilizidi kumpenda hasa katika uwajibikaji wa kazi, pamoja na kalama aliyojaliwa ni uchesi na utoto mwingi uliojaa akili.

Leo Mrs Mishoki alimkuta Gorii” akiwa chumbani Kwake akiwa na picha ya Mamake, baada ya kumuona Mama ilibidi aifiche ile picha ila mama alikuwa amemuona muda, alimua kukaa kimya kama hajaona

   “” Gorii” Unajua leo tunao wageni! Kaka zako wawili wanakuja likizo! Naomba twende wote sokoni tukatafute mboga!”

   “” Na Bibi je?”

   “” Unavompenda Bibi yako! Kwani wamkimbia?”

  “” Gorii alitabasamu huku akisimama waondoke.”

  “” Wapi tenaa waenda!?”

  “” Ngoja nimchungulie Bibi kwanza! Huenda anataka zawadi ya kutoka nje!?”

Muda huo Rich nae alitokea huku akimuita Gorii”.

   “” Gorynah”.. muda bhana! Leo hujui kakazangu wanakuja! Humu ndani sikuzote Mimi ndie dume pekee! Sahii nitakuwa situmwi ovyo! Kina Kaka nao watawajibika.

   “” Aaa..! Na wewe Ka Rich..!! Nilikuwa namuaga Bibi kwanza! Halafu kumbe na Wewe waenda!?”

  “” Unaweza kubeba mizigo yote mkihemea!?”

Mama ilibidi awakatishe make wakianza kuhojiana huwa hawamalizi.

   “” Nyie watoto tuondoke bhanaa!”

Wakiwa sokoni walihemea vitu vingi, Gorii” na Rich ndio walikuwa wakusaidiana kubeba na kuweka kwenye gari.

 

Baada ya Kumaliza ilibidi waanze kurudi. Wakiwa njiani Goryanah ” alimuuliza Mamake Rich.

   “” Mama mbona vitu vingi hivyo umenunua si vitaharibika? “” Yaani huko kwetu huwa twaenda na mfuko wa magufuri wa mia mbili vitu vyote vyatoshea, siku nyingine huwa nakimbia gengeni bila mfuko naleta nyanya, kitunguu, ndio kwisha hapo! 

   “” Hi ni familia kubwa, kukaa twaenda kuhemea kila siku sio vizuri! Huwa twahemea vitu vyakukaa navyo siku nyingi! Muda mwingine ni mazingira tu ndio unachagua kipi ufanye!”

   “” Aaah!! Ndoo… maaana!” ” Kule kwetu unajua hata tukipika mboga huwa ni moja tu! Huku Sasa yaani vitu vingi mpka huwa nashidwa nianzie wapi!? Ila Mimi vyote huwa naonja!”

Mama ilibidi acheke tu… Mtoto hajui kuvunga.. Rich nae aliamua kumvuta nywele kwa nyuma huku akimcheka.

   “” Halafu Rich umenikumbusha! Utampitisha dadako saluni leo mpendeze, si unamjua Jolvin huwa hapendi uchafu ataanza kuwasema huyoo!”

   “” Jolvin… Itakuwa ni huyu mjukuu wa Bibi muda wote huwa anamuongelea Sana! Jolvin, Jolvin… Oooh! Kwani yeye msafi?

Gorii Alihoji, lakini Rich aliwahi kumjibu.

   “” Ni msafi huyo! Itabidi leo nitaenda kukuonesha chumba chake ukijue! Yaani kila kitu cheupe pee!”

   “” Haaaa! Atakuwa na majini huyo, kijijini kwetu mtu akiwa msafi zaidi! Itakuwa anakaa na jini Safi.”

   “” Wewe Gorii” tulia Basi akikusikia hivyo kakako atakuuliza!? Acha niwaache saluni muwahi kurudi Sasa

Mama aliwashusha pale, Kisha aliwaachia pesa kidogo watumie. Ile kushushwa tu! Gorii” alijinyosha huku akitizama mji ulivyojaa majengo mazuri alicheka kwanza Kisha alishusha pumzi ndefu!

 

   “” Unajua Nini Rich… Afadhari leo tutembee tembee,, yaani kwenu kila ukitoka ni kwenye gari! Twende Tandale kwanza..! Huko Kuna saluni za bei nafuu!”

   “” Goryanah umeanza… Mama kasema tuwahi kurudi! Mimi huko uswahilini sitoenda!”

   “” Hutoenda wakati pesa nimekabithiwa Mimi! “” Ayaa hiace hiyo hapo ya Tandale mi napanda ka unabaki.. we baki”

Rich hakuwa mjanja tena ilibidi akubali! Make hata pesa ya nauli hana Walifika Tandale wakawa wameshuka.

   “” Twende kwenye hio saluni.. huenda wanae bei nzuri.

Baada ya kufika Gorii” aliulizia….

 “” kusuka yebo bunda tatu shi ngapi?”

  “” Elfu kumi na tano tu!”

  “” Hapana hela nyingi mno hiyo!! Nikajua elfu nane!!”

   “” Dada.. nenda kwenye saluni yako uliyoizoea naona umekosea saluni.

Msusi mmoja alimjibu, make Kama anamletea mazoea kwenye kazi yake.

Huku kwa Rich yeye hana mbavu, make alikuwa akisikiliza jinsi wanavyoelewana bei.

   “” Vipi mbona unacheka.. Ndio umefurahi!? Ila wana bei kubwa mno! 

   “” Gorii” nacheka kwasababu unaulizia kusuka yebo,, nywele ya kishamba hiyo hata demu wangu hawezi suka hiyoo..!”

   “” Ooh! Kumbe Rich huwa unafanya tabia mbaya! Kumaliza form four tayari unae dem?”

   “” Wewe unashangaa Mimi!!?’ ” wakati ninae rafiki yangu anae Mtoto!?”

   “” Itakuwa huyo ndie kakufundisha tabia mbaya! Ndio maana upo kwenye mahusiano ukiwa na umri mdogo!”

 

   “” Kwani Wewe bado!!?”

 

   “” Bado Nini!? ” Mimi Sina tabia Kama zako!”

Rich alibaki kumcheka kwanza Kisha alimshika sikio.

   “” Wewe si una miaka Kama yangu..? ” ushakuwa mbona!!”

   “” Twende bhana Saluni nyingine naona wataka kuongea!!”

   “” Nijibu kwanza…. ndio twende.. Ukipata mchumba huwezi olewa! Make tunalingana kila kitu!.

  “” Unafurahisha Sana Rich, Mimi nawaza nipate pesa! Mamangu nimjengee nyumba nzuri! Wewe wazani siku zote Mimi nitaendelea kuishi kwenu?”

Rich ilibidi akae kimya kwanza, Huku akimfikilia Gorii” atakuwa ni muongeaji Sana lakini kutimiza malengo yake ni changamoto kwa mtazamo ule hata hiyo pesa ataitoa wapi?

Walielekea kwenye saluni moja ilibidi akubali kutumia gharama ya ishirini na tano, Rich alimshawishi abadilishe mawazo ya kusuka na sio yebo tenaa!

Baadae walirudi Nyumbani huku wakiwa wamenunua vyakula vya mtaani, Goryanah alipitiliza moja kwa moja Chumbani kwa Bibi, alitoa vile vyakula akaviweka mezani.

   “” Bibi! Leo nilienda kuzurura huko nje! Nimepata vyakula vya mtaani kwetu! Nikaona nikuletee wewe kama unavipenda Karibu tule!”

Rich aliingia, Kisha alikaa mezani nakuanza kushambulia ile mihogo, Bibi nae akasema awee!! Sio ya kukosa alianza kula huku wakifurahia kwa pamoja.

   “” Wewe Rich! Mbona unaivuta vuta hivyoo!?”

   ‘” wewe nifate kwanza! Si nilikwambia nitakuonesha chumba Cha  Jolvin.”

   “” Ooh! Nipeleke kwa huyo Kaka mwenye vitu vyeupe!”

Waliongozana hadi kwenye hicho chumba baada ya kufika, Rich alifungua mlango! Kweli chumba kilikuwa kinavutia, kitanda kilitandikwa vizuri!

   “”Waoo!! Chumba kizuri sana

Goryanah aliongea huku akijitupia kitandani.

   “” We wee!! Dada wa kazi kamaliza kufanya usafi sahii tu halafu Wewe wavurugua kitanda! Hivi kumbe wajua kingeleza!?”

   “” Na ningesoma Wewe huniwezi kwa kuongea kingeleza!”

   “”Ayaa tandika vizuri tuondoke!  nimesikia wamefika Airport! Tusikutwe humu.

Walifika sebuleni huku Gorii” aliingia jikoni kuwasaidia wapishi, baada ya kumaliza walileta mezani! 

Muda huo Jolvin alikuwa akiingia huku akiwa na wenzake wawili wakipiga stori!

   “” Hodi humu Ndanii!!!”

Jolvin alibisha hodi Kisha akafatia Esau na Joely.

  “” Daaah! Wanangu mmependeza kweli..!”

Mama alifika kuwapokea huku akifatia Rich, Kakake walimpenda Sana hutaamini wote walimkumbatia huku wakielekea sebuleni.

   “” Bibi yupo wapi maama!?”

Jolvin Alihoji huku akijaribu kumuita Bibi yake.

   “” Atakuwa bafuni, si unamjua Bibi yako anataka arudi ujana Kama wewe!”

   “” Goryanah… Chakula bado tu! Mje msalimie wageni kwanza.

Mama Aliita.

Neno Gorii” lilikuwa jina geni kwa Jolvin, Esau na Joely ilibidi watoe macho kutizama Gorii” mwenyewe anaeitwa.

Wakati wakiwa jikoni wadada wa kazi wote walishadadia Gorii” apeleke kinywaji kwanza kwani wote wanamuogopa Jolvin, muda wote ni kusodoa, wakati mama anaita Goriii ndio alikuwa akimimina Juice kwenye Grass baadae alifika sebuleni na kuweka mezani.  Nini kiliendelea Usikose Sehemu ya sita 

Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya Goryanah Kumtumia Chochote

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM 

Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii editor@kijiweni.co.tz  

 

14 Comments

  1. Rumbyambya Jr on

    Kwa vile Jana hatukupata nafasi ya kuisoma leo ziwe 3 na Sio mbili Admin sema haka ka story mbona kama Jolvin atampenda Gori

Leave A Reply


Exit mobile version