Ilipoishia ” Mudy baada ya kumfikia ilibidi asimame nyuma yake make alikuwa amenuna. Goryanah ndio anageuka huku akipaza sauti, ndipo anakutana na Mudy uso kwa uso ilibidi hasira zishuke Kisha alicheka tu.

“” Hapo sawa’ make nilikuwa naenda kukufokea vibaya! Harafu leta hizo pesa ulizokusanya make Kuna vijana hapa nimeona mtu mmoja akirusha jiwe upande wa pili naona Kama wanashituana hivi! Hawa wanahitaji pesa, fanya hivi wewe kaa utulie.”

Endelea 

SEHEMU YA PILI-02

   “” Lakini Gorii”

  “” Tulia bhana.. ushaanza kuitana bila sababu..! Nipe haraka hizo pesa!”

Mudy ilibidi afanye vile, Goryanah alizihifadhi vizuri zile pesa Kisha alipaza sauti..

   “” Kama mna nguvu si mjitokeze! Najua ni wewe Hammad na group lako! Harafu hivo vi barua unavokuwa wanitumia sivitaki.”

Mtu nne zilitokea chemba huku zikiwa na malungu zikiongozwa na Hammad Kama kiongozi wao.

Goryanah baada ya kuwaona ilibidi amfuate kiongozi wao.

   “” Lakini Hammad.. unafanya haya yote ni kwasababu ya kutaka kunioa tu! Wewe ni mkubwa kwangu wanizidi miaka mitatu! Huoni Kama utafungwa na serikali Mimi sijatimiza miaka kumi na nane!

Hammad alimsogelea Karibu huku akimtizama machoni, Kisha alinyanyua mkono wake akishika nywele ya Gorii” iliyokuwa imefungwa nywele ya uzi, alifanya kunusa mkono wake Kisha alitema chini.

   “” Wewe ni binti mrembo sana! Sema ni vile huelewi tu! Nikikuoa Mimi hutakuwa ukinuka jua!”

 

Goryanah ilibidi acheke kwanza Kisha alimshika kichwani akikagua nywele zake.

   “” Kama ni kunuka jua, naona mwezi huu ndio mwisho! Huoni dalili za mvua zimeshaanza tayari!? Wewe ni msomi lakini hujui Kama dalili ya mvua ni mawingu!”

Hammad alitazama juu kwanza, kweli kunae dalili ya mvua alitabasamu Kwanza kisha alisogea Karibu alimnong’oneza sikioni.

   “” Kesho ni birthday yako unatimiza miaka kumi na nane! Hiki kipinganizi Cha kusema utimize miaka kumi na nane! Kwasasa familia yangu naenda ishilikisha ije kuposa kwenu!”

  “” Hata iweje… kamwe sitaolewa na wewe! Mimi kwasasa sinae mpango wa kuolewa nataka nitimize ndoto yangu kwanza, nataka mamangu aishi mazingira mazuri!” Hammad aliamua kuondoka na kikosi chake.

Huku kwa Goryanah Alibaki akimtizama Hammad mpaka anaishilia.

   “” Gorii!! Kipi waenda kukifanya naona jamaa amekuganda kweli! Lakini hamna huwezi ukaolewa, wewe bado ni binti mdogo Sana!”

Gorii Alibaki akizunguka kutafuta namna ya kufanya

   “” Sasa Mudy! Kuna kitu nimewaza! Unaonaje nikitoroka Nyumbani nikaenda kufanya kazi za ndani mjini! Nahisi hapo hataniona!”

  “” Mimi je? Utaniacha na Nani?”

  “” Aaah! Wewe utabaki na mama pamoja na mamangu nitakukabizi umtunze!”

  “” Hapana sitaweza! Mamangu Mimi ananichanganya kumhudumia iweje mamako mzazi!”

  “” Ooh uu! Sasa nafanyaje!?

  “” Twende Nyumbani Kwanza!”

Huku Nyumbani Mamake Goriyanah alikuwa akifanya usafi, baadae Simu yake ilipigiwa ilibidi apokee Simu Huku akiangaza upande wa pili, ilionesha ni Simu ya Siri.

  “” Nimekwambia nakuja! Ila ngoja Kwanza Gorii aje!

Muda huo Gorii anafika Huku akiwa na kelele akipiga beseni lake Kama ngoma.

   “” Maamaa! Mwaka huu tunaondokana na umaskini! Leo nimeuza mboga zote.”

Mama baada ya kusikia vile alikata simu haraka Kisha aliiweka mezani.

“” Ooh binti yangu Gorii” kauli yako moja to ndio imebaki ni kuondokana na umaskini!”

Gorii alifungua pesa kutoka kwenye mkoba wake Kisha alimpatia Mama, Mama alipokea zile pesa Kisha alitabasamu Kwanza huku akiongea moyoni.

   “” Hizi pesa haziwezi kuuondoa umaskini! Hivi ni vi shilingi tu! Lakini hongera kwa kuwa unazidi kupambana!”

   “” Mamaa! Mbona kimya hujapenda? Halafu nina njaa..!””

Ilibidi waingie ndani wapate kula, muda huo Simu ya Mamake iliita, Gorii ndie alikuwa wa kwanza kuiona make ilikuwa upande wake, alichukua Kisha alitizama mpigaji aliona imeseviwa “” Mzee Rajab” ilibudi amtizame mamake kwanza huku akiwa na hasira.

   “” Maamaa! Si uliniahidi hautawasiliana na Mzee Rajab!? Mbona anakupigia simu?”

Mama Alibaki na wasiwasi huku akimtizama binti yake, ilionesha hafurahii mahusiano yake kabisa na Mzee Rajab!

Goryanah aliamua kuondoka huku akimuacha mamake sebuleni, alielekea bustanini kunyunyuzia bustani! 

   “” Mama Kila siku ni yeye na Mzee Rajab! Mzee mwenyewe kachoka kweli nasikia anae TB mama kamganda kweli nahofia siku moja nitampoteza!”

“” Gorii”

Mama aliita alitoka kumfuata binti yake!

“” Wewe nenda tu! Nimemuona Mzee Rajab anakusubili kule mnakokutaniaga!”

 

Mama alipigwa butwaa Kwanza Kisha alitazama upande wa pili ndio anamuona Mzee Rajab! Akimpungia mkono ilibidi apunge na yeye!

Mambo yote Gorii alikuwa akitizama, aliamua kumruhusu mamake aende japo hakupenda kuona hivyo!

Baadae aliingia ndani huku akikusanya nguo zake na kuweka kwenye sarfet, baada ya kumaliza ilibidi ampangie mamake nguo kwenye begi huku akiamini siku akiondoka itabidi waongozane wote kwenda mjini na hapo ndio atamkomboa mamake kutoka kwenye mikono ya Mzee Rajab!” 

   “” Hapa Mama lazima umuache Mzee Rajab ukaanze maisha mapya mjini!”

Siku hiyo Gorii alibaki kumgonjea mamake asimuone tangu aende kwa Mzee Rajab! kiza kilianza kuingia ilibidi ajiandae kulala.

Lakini alikumbuka Kuna kiakiba alikuwa akikiweka chini ya kitanda ilibidi abinue Godoro aangalie! Alijaribu kukagua lakini hakuona mwisho kabisa aliona mfuko umeanguka chini aliuchukua na kuufungua! Alikuta Kuna makopo ya dawa Kama manne ilibidi afungue ndio anakuta kunae vidonge vikubwa! Alifunika kwanza Kisha alipiga kelele huku akisema…

   “” Tayari mama ana TB ya Mzee Rajab!!!!?”

Mwisho alijikaza tena Ili afungue kopo la pili, baadae alifungua alifunga huku akiligeuza upande wa pili ndio anaona limeandikwa HIV ilibidi arudie tena japo alikuwa na elimu ya Darasa la Saba nayo ilimsaidia kuelewa.

Kwa ujumla alithibitisha mamake ni muathirika ilibidi akae chini kwanza huku akilia, baada ya kumaliza kulia wazo likabaki je atamuuliza Mamake Kama ni Muathirika? aliamua kurudisha zile dawa kwenye mfuko Kisha alirudisha sehemu yake!

Wakati anarudishia Godoro ndipo anaona ile pochi aliyokuwa akiwekea akiba ipo chini, aliifungua lakini hakukuwa na pesa tena, hapo hapo hasira ndio zilizidi kumjaa akiangalia ndio akiba alotegemea itawapeleka mjini wakapange chumba lakini mamake kaikwapua, akili ilimuijia alijua ni Mamake kaenda kumhonga Mzee Rajab kwasababu ni tabia yake amekuwanayo toka mwanzo.

 

Alichukua rungu huku akikata mtaa kuelekea kwa Mzee Rajab! Amweleze hizo pesa anazomuomba mamake atakuwa kapeleka wapi?

Baada ya kufika, Aligonga mlango ndipo anatokea Mke wa Mzee Rajab! Na yeye baada ya kumuona Gorii, ilibidi aingie ndani Kisha alitoka na Rungu na yeye huku akianza kumkimbiza.

   “” Wasimbe nyie! Mamako amebaki kula pesa za Mume wangu halafu unakuja kumtafuta Mamako kwangu! Nakwambia na huyo mamako anaendeleza umalaya na waume za watu! Chakula chenyewe ni ugali mboga mboga! Jumlisha hivo Virus sahii tu unaitwa yatima kwa umalaya wa mamako, tena nakupa pole!”

Gorii” alikuwa akikimbia baada ya kusikia Maneno ya Mke wa Mzee Rajab ilibidi asimame huku akiamini kumbe kweli mamake ni Muathirika, hapo hapo alianguka chini akazima.

   .. .. Itaendelea Usikose Sehemu ya Tatu ….. 

Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

Mpe Nguvu ADMIN Kwa Kumtumia Chochote

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM 

Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii editor@kijiweni.co.tz  

18 Comments

Leave A Reply


Exit mobile version