Ilipoishia 

Alimsogelea Karibu Kisha alimnong’oneza sikioni.

   “” Ukinigusa Mimi ndio umegusa familia nzima ya Mishoki! Kwahiyo kuwa makini!”

Hammad alisogea nyuma kidogo Kisha aliwapatia Ishara wenzake kilichofuata hapo ni kelele tupu huku wakipeana vipigo vya kufa mtu, baadae Hammad aliwanong’oneza wenzake wakatoka haraka haraka .

Endelea 

SEHEMU YA NANE 

 

Huku barabarani Jolvin alikuwa na Anelisa wakiendelea kula bata, siku hiyo walizungukia mitaa mingi, Kama bahati nzuri walifika sehemu Kunae kelele ilibidi wachungulie kwa pembeni alimuona Kama Rich amelala ilibidi ashuke, pembeni kidogo alimuona Gorii” katapakaa tope mwili mzima huku akizidi kumlalamikia Hammad ambae nae alikuwa hoi, alikuwa amelala chali huku akimtizama Gorii” kwa pembeni akiongea nae.

   “” Kwanini nisikuoe tu Gorii” tukaachana na mambo haya ya kuaibishana mtaani!?”

   “” Kwanza hufai kuwa mme! Mara hii tu nimenusurika kumwaga ubongo! Hio nguvu ya kuitwa mke wa Hammad itatoka wapi!?”

Huku kwa Rich ndio alizidi kulalamika, ukiangalia mwili wake laini laini alipigwa rungu moja tu hoi akiugumia maumivu. Alimtizama Gorii” ambae nae yupo hoi.

   “” Sasa Gorii” hapa tunaondoka vipi!? Mimi mwenyewe hata nguvu Sina za kusimama! Ee Mungu saidia Kaka White asituone tulivyofanana na ardhi make atatuongezea fimbo tenaa!”

Gorii” ilibidi ajikaze alisogea Hadi kwa Rich Kisha alifanya kumuinua, akimkalisha.

   “” Yaani leo tumekuwa Kama watu wa mazingaombwe si sura zetu , nguo zetu! Hivi na Mimi nipo Kama Wewe usoni!?”

   “” Wewe ndo kabisa!! Yaani hiyo nywele kung’aa labda ukadumbukie ziwani!”

 

Walicheka kwa pamoja, Hammad nae aliamka ilibidi avute Simu huku akiwapigia rafiki zake, kumbe muda ule aliwarusu wakaandae mazingira Nyumbani! Alijua lazima Gorii” akubali kuongozana nae, make ile pesa hawezi kuilipa.

 

Muda huo Jolvin alikuwa akiwatizama vizuri! Hakuelewa kipi kilikuwa kinaendelea pale! Muda huo kumbe alikuwa amewapigia Simu kina Esau na Joely wakawa wamefika pale!

Walishuka kwenye gari haraka, hutaamini wote walikimbilia kumuona Rich, halafu Gorii yeye walimtenga. Gorii” hakujali walaa!” alibaki akijitengeneza vizuri ili ainuke lakini mguu wake ulikuwa umeteguka ilibidi akae chini huku akijaribu kuunyosha! 

Muda huo Jolvin alikuwa akimtizama, Kisha alitingisha kichwa huku akiongea mwenyewe.

   “” Sijui lini ataipata familia yake akaepukana na kudhalilisha familia ya Mishoki! “

Huku kwa Hammad baada ya kuiona ile familia imetia timu pale ilibidi akimbie, lakini Jolvin alikuwa amekalili prate namba ya gari iliyomchukua, swala la kuanza kupigishana kelele na mtu mchafu haina maana Kwake!”

Rich aliinuliwa na ndugu zake wawili huku kwa Gorii” alijua leo ndio siku ya kuwa mbali na familia ya Mishoki, alibidi aanze kuandaa mazingira ya kuwa mwenyewe.

Alishangaa Kuna mtu kamnyoshea mkono anataka kumsaidia, alimtizama kwanza asiamini Jolvin ndie yupo pole, alitazama kwanza mikono yake ilivyochafuka na tope! Ikabidi atikise kichwa kukataa, lakini Jolvin aliendelea kumnyoshea mkono.

Ilibidi atoe mkono wake huku akiangalia jinsi Jolvin anavyomshika mkono, japo alimshika kwa kinyaa Sana ila ndio ulikuwa msaada Kwake.

Alimkokota taratibu kuelekea kwenye gari ya Kina Esau make yeye alikuwa na usafiri wake na Anelisa, alimkabizisha kisha alirudi kwenye gari yake! Ile anafika tu Anelisa alikuwa ameandaa maji ya chupa aliamua kumnawisha kwanza huku akimuuliza.

   “” Huyo binti ni Nani katika familia ya Mishoki!? Imekuwaje ukubali uchafuke kwaaajili yake!?”

   “” Achana nae kwanza! Hakili yake haipo sawa’ ndio maana nimemsaidia! “” Muda nao umeenda kweli Ngoja nikupitishe Nyumbani kwanza.”

 

   “” Hutaki kuwasalimia wazazi!!?”

   “” Ni usiku sahiii! Nitakuja mchana, Ngoja nikawawahi kwanza hawa wapuuzi!”

Huku Njiani Esau ndio alikuwa akiendesha gari! Joely yeye alikuwa Hana mbavu! Muda wote alikuwa akiwapiga picha Kama kumbukumbu.

   “” Hapana Kaka! Usiipost… Nitaabika ujue!”

   “” Hivi bado unae Sophia! Nataka picha hizi nimuoneshe!”

Gorii” muda huo yeye alikuwa katulia huku akimfikilia Hammad anavyozidi kumfatilia, zaidi alimuwazia mamake alichukua pesa nyingi kwa matibabu gani? Alijikuta akianza kulia mpka wenzake wakashituka.. 

“” Gorii” Nini tenaa!? Mmepigana kule, ulikuwa hulii sahii ndio walia, au umeumizwa Sana!?”

“” Mamangu kachukua pesa ya matibabu! Ile ni pesa ndefu nawaza atakuwa kazidiwa Sana! Sijui hata anatibiwa wapi!? Kesho itabidi nirudi kumtafuta Hammad huenda anajua wapi mama alipo!”

Wote walibaki kumtizama kwa makini.

   “” Lakini Gorii” usiwaze mama atakuwa salama tu! Nimeona machapisho yako mengi yamejaa mtaani! Lazima yatamfikia tu!

Walifika Hadi Nyumbani kilichofuata, Gorii” na Rich walishuka wakawa wamekaa nje kwanza.

   “” Vipi mbona hutoki Mimi nataka kuoga kwanza!”

Rich aliongea Huku akitaka kuingia kwenye maji, Gorii” ilibidi akakae getini kwa walinzi akingoja Rich aoge kwanza!.

Muda huo huo Jolvin ndio anaingia, alifika getini kwanza Kisha alishusha kioo kumtizama Gorii”. Aliamua kupaki gari pembeni Kisha aliingia ndani kubadilisha nguo baadae alirudi akiwa na Bibi.

   “” Umemuona Mjukuu wako wa kufikia alivyofananania na ardhi!?”

 

Gorii” alipomuona Bibi yake alikimbia kwenye swimming pool! Alijitupia ili kuepuka aibu! Ile Bibi anakuja kutizama aliona maji ndio yanaruka ilibidi wote wabaki wakishangaa.

Huku kwa Rich baada ya kumuona Gorii kaingia ilibidi apige kelele make alikuwa na nguo ya ndani tu!

   “” Wewe hebu tulia bhana! Mi hata sikuchungulii!? Si ukae pembeni na Mimi nikae hii pembe!”

Bibi Alibaki kucheka aliamua kurudi ndani.

Jolvin yeye aliamua kusogea Karibu Ili azidi kuwakagua Kama wanatakata kweli.

   “” Ayaa! Wewe binti mwenye nywele ndefu inuka tukuone!!”

Gorii” aliinua kichwa.

“” Bado kabisa hujatakata! Sogea hapa uchukue sabuni!

“” Sasa nasogea vipi wakati Rich yupo sehemu hiyo!?”

“” Rich zama chini mwenzako asogee!!”

“” Hapo sawa’ umeanza kutakata!”

Baada ya kumaliza kuoga, kazi ikabaki kwa Gorii” atatoka vipi wakati tayari nguo zimeloweka.

   “” Kaka White!! Zima Basi taa mi nikimbie ndani kubadilisha mavazi!”

  “” Sahii unaogopa! Wakati mpaka Sasa upo na mwanaume kwenye maji Kama ni kuchunguliwa tu! Ushaonwa!?”

   “” Kaka White! Niitie Basi Dada” aende chumbani kuniangalizia nguo!” Nahisi baridi et..!”

Jolvin alipiga Simu, nguo zikaletwa ilibidi waondoke wamuache mwenyewe!

Gorii” ndio akapata muda wa kwenda chumbani kubadilisha hata hivo ni usiku Tayari.

Baada ya kumaliza Bibi alimuita chumbani Kwake! Alimsaidia kumnyoosha nywele huku akimuulizia kipi kiliwakuta ilibidi amwelezee, hata hivyo huwa hamfichi.

   “” Kwahiyo ni laki mbili tu ndio inatakiwa!?”

  “” Ni hiyo tu! Halafu Bibi naomba umuombe mama aniruhusu nifanye kazi ili niweze kumlipa Hammad pesa yake!”

   “” Hio ni pesa ndogo Sana! Nitakulipia mjukuu wangu!”

  “” Bibi unazo hizo pesaa!!?”

Bibi alicheka Kisha alimuaga akalale kwanza, kesho ataongea nae. Ile ametoka tu! Bibi alimpigia Simu Jolvin alipofika akaanza kumuelezea kuhusu Gorii”.

  “” Usijali Bibi! Mimi nitaenda kuilipa hiyo pesa! Kuhusu Hammad nitaongea nae! Na hatomgusa tena Gorii”.

Siku iliyofuata! Majira ya mchana Gorii” alikuwa kajipumnzisha chumbani Kwake huku akimfikilia Mamake atakuwa wapi! 

Jolvin Aligonga mlango kwa Gorii” akawa amefungua. Ilibidi kwanza akusanye zile karatasi akaziweka vizuri.

   “” Sa mbona unakubali kuchafuka tope! Wakati chumbani kwako unapangilia vizuri!”

   “” Kaka White!! Leo umeingia chumbani kwangu! Itakuwa Kuna shida ee!”

Jolvin  alisogea karibu mezani Kisha alichukua picha ya Mamake Gorii” akaitizama, huku akichukua karatasi alizokuwa kachapisha.

Gorii” alibaki amesimama Karibu na mlango, Jolvin alimuuliza.

   “” Kwanini hukai! Au waniogopa!?”

   “” Ni Juzi tu umenifungia chumbani! Leo tena tupo wote chumbani Mimi sikuamini!”

Jolvin alifanya kupotezea, aliinyanyua Simu yake akawa amempigia Hammad Kisha alimpatia Simu Gorii” aongee nae!

 

   “” Gorii” naomba unisamehe kwa kile kitu kilichotokea Jana! Pia kuhusu Hilo Deni la mamako tayari Bibi yako kalipia! Kwasasa upo huru!”

Jolvin aliidaka ile Simu Kisha alimalizia kuongea.

   “” Usajili wa Prate namba yako tayari upo kituoni! Kama unafanya tukio baya kumbuka maovu yako yametangulia kituoni.”

Kisha alikata Simu. 

“” Kaka White! Thank you!”

Jolvin alimwangalia Kwanza Kisha alicheka make anapenda kingeleza huyu.

     “” Sorry lakini, elimu yako umesoma Hadi ngazi ipi!?”

“” Ngazi tenaa? Au Unamaanisha Darasa la ngapi? Mi nimeishia Darasa la Saba! Nikawa nimefaulu kujiunga kidato Cha kwanza, sema shule ilikuwa mbali ilikuwa inanilazimu nikakae huko! Na Mimi kumuacha mama pekee siwezi, ilibidi nisiendelee na masomo! Japo niliahidi kuwa Karibu na mama muda wote nimlinde lakini sinae tenaa!”

Gorii” aliongea maneno mazito, kweli alimpenda Mamake hata kupambana kote ilikuwa ni kwaajili ya Mamake.

   “” Pole Sana! Mama atarudi tu! Hata Mimi nitakusaidia kumtafuta! Vipi lakini mbona Kama unashinika uso unae maumivu kwenye bega!?”

Gorii” ilibidi akatae japo alikuwa ameumia kwa kupigana na Hammad.

“” Najua unanificha Basi niruhusu nijilizishe Kama kweli hujaumia!?”

Jolvin alimsogelea Karibu Kisha alishusha shifoni alokuwa kavaa, aliona ni kidonda kibichi bado kinatoa damu kutokana na ile nguo alokuwa kavaa ilikuwa imeshika kwenye kidonda.

   “” Naomba utoe hio nguo ya juu Kisha jifunge kanga! Nakuja mara moja na dawa!”

Alienda Hadi chumbani Kwake akarudi na boksi la huduma ya kwanza! Joely akawa amemuona ilibidi amfuate mpaka anafika!

 

   “” Upo tayari niingie?”

Gorii” alimruhusu muda huo alikuwa kajifunga kanga kifuani.

   “” Najua itauma ila jikaze ili upone haraka!”

Joely nae aliingia, akifatia na Rich.

“” Gorii” kumbe wewe uliumia hivo Jana! Mbona ulijikaza tu! Uwe unasema kwanza! Utakuja kuoza eti..!!”

Jolvin, Esuu walibaki kumtizama Rich, mpaka walicheka. 

Jolvin alimwangalia Joely Huku akimpatia ishara ampake dawa make yeye ashaanza kumuonea huruma kwa ile dawa ni Kali sana, ilikuwa ni ” iodine solution”

Joely alichukua pamba akainoweka kidogo kwenye dawa Kisha alifanya Kama anamfuta, Kelele ya maumivu ya dawa ilisika nyumba nzima! Nini Kitaendelea ? Usikose Sehemu ya 09

Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya Goryanah Kumtumia Chochote

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM 

Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii editor@kijiweni.co.tz  

21 Comments

  1. Jjb-hsnf-fdk on

    Simuliz ni nzuri
    Japo sehem ya rich kukutana ns Goran haijaeleza vizuri wakati tuliona rich aliaga kwa mama ake akaondoka nyumban bila kumuaga Goran

  2. Story ina maana kubwa… Gorii. Ni maskini lkn anapambana. Na family ya mishoki inampa imani Gorii.. Kwani wanamjali sana. Hongera sana mtunzi.

Leave A Reply


Exit mobile version