IipoishiaAlifungua mlango Kisha akarudi kitandani, alimsikia Jolvin akimwelezea Doctor.

   “” Ni tumbo la ghafra tu! Limemkamata ameteseka kweli! Nimemkuta kitandani akiweweseka kwa maumivu! Fanya umsaidie haraka Doctor! Akipata nafuu Kuna sehemu naondoka itabidi niende nae Kama khari haitabadilika, na hii ni kwa usalama zaidi 

Endelea 

SEHEMU YA KUMI NA TANO

 

Doctor alimuasha Gorii! Baadae alimuuliza.

  “” Kichwa kinasumbua pia? Halafu unaonekana Kuna Jambo linakusumbua, mapigo yako ya moyo yapo juu Sana!”

Alimaliza kupima akamgeukia Jolvin ili ampatie majibu!

   “” Mgonjwa wako anaonekana mapigo ya moyo yapo juu! Na ndio imechangia kuumwa na kichwa! Kaa nae vizuri huenda ana stress ndio inachangia awe hivi! Kuhusu tumbo huwa ni kawaida ya wanawake wakikaribia kwenye siku zao wengi wao huwa wanaugua, ila utampatia dawa za maumivu atakuwa sawa!”

Doctor alimaliza kuongea huku akichukua vifaa vyake akisindikizwa na Jolvin!

   “” Oooh!! Afadhari nimesalimika! Hapa Kaka White hataondoka kwa khari hii!”

Jolvin alirudi huku akiwa na sahani ya chakula aliweka mezani.

   “” Unaweza ukatembea hadi mezani!?”

Gorii alifikikilia Kwanza Kama atasema ndio, Jolvin atajua anaendelea vizuri ilibidi asingizie mwili hauna nguvu. Jolvin ilibidi amletee huku akimshikilizia sahani ale, baada ya kula alibaki amekaa pale huku akiangalia simu yake masaa yanazidi kwenda.

   “” Unachelewa kwa Anelisa!!?” Gorii alimuuliza.

   “” Aa aa! Unajua Anelisa anaumwa ilitakiwa nikachukue dawa kwao nimpelekee! muda nao unazidi kwenda sijui hata nafanyaje!?”

Gorii ndio anageukia upande wa pili huku akivuta shuka, akiambatanisha kikohozi Cha kutafuta baada ya kujua Jolvin bado anawaza Safari..

“‘ Goryanah!! Usilale basi! Kaa tuzungumze basi simama nikwambie!”

Simu ya Goryanah iliita alikuwa ni Bibi, Jolvin aliwahi kuipokea.

   ‘”‘ Bibi bado hajawa sawa naona anazidi kukohoa! Ila nimempatia dawa Wewe usijali endelea na kazi Mimi nitamhudumia.”

Baada ya kukata, simu yake ilipigiwa na Anelisa, alibaki akimtizama Gorii make mlio wa simu yake ulisikika, Gorii aliamua kumjibu.

‘” Kaka White!! Naona Kama nakusumbua Wewe nenda tu! Nitakuwa sawa! Hata hivyo Mamangu alipenda kuniambia nikiugua lazima niyazuie maumivu hata kwa kufanya kazi kuliko kulala! Hapa nataka nifue fue nguo zangu! Naamini nitakaa sawa”.

“” Hapana Gorii! Wewe unaumwa hauwezi ukalazimisha ukafanya kazi ngumu! Basi Mimi nitashinda na Wewe siku mzima, kwa Anelisa sitaenda tenaa, si unaweza kujiandaa twende wote sehemu! Jana wakati natoka pale Kuna nguo ulivaa ukapendeza Sana niliamua kuichukua basi utavaa hiyoo! Ila umepona Kwanza make ninakokupeleka kunae makelele!?”

Gorii baada ya kusikia kaailisha Safari ya kwenda, huta amini alijisau kabisa Kama ni mgonjwa aliamka na kukaa huku akimtizama Jolvin! 

 “Dakika tano tu nimemaliza kujiandaa”

Jolvin alitoka anacheka, aliingia Chumbani Kwake akamletea gauni Kisha alimsubili sebuleni. Baada ya Gorii kumaliza kuoga alivaa ile gauni ilimtoa vizuri! Ikamfanya hata Yeye asikatike kwenye kioo muda wote ni kujigeuza geuza mithili ya kambale awapo kwenye maji, Alianza kutembea kwa madaha taratibu Kama umemuona Afisa masoko toka Bank akishuka ngazi!

Alitoka taratibu huku akichungulia Kama kunae watu sebuleni, baada ya kujilizisha ndio alipita taratibu hakutaka hata wadada wa kazi wamuone! Alipiga hatua Kama mbili ndio anasikia sauti ya kidume ikimuita alibaki kasimama huku akimsikilizia afike.

   “” Waoo ur so beautiful! Yaani umependeza sana., Kisha alimshika mkono kuelekea kwenye gari!”

Walipanda gari kuelekea kwenye hotel moja! Siku hiyo kulikuwa na Sherehe ya mwanafunzi mwenzake na Jolvin kutimiza miaka kadhaa. Kuna wanafunzi wengi walikuwa pale!

   “” Kupendeza umependeza ila usiniaibishe! Naomba ukae sehemu moja halafu tulia na Mimi!”

Gorii alibaki kumtizama tu, Kisha alivuta kiti akakaa! Walichukua vinywaji huku wakiendelea kuangalia maigizo mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea mbele.

“” Gorii.. !! Jolvin alimuita.

“” Aa Kaka White! Wanafanya maigizo mazuri! Mwangalie yule mkaka kachukua uhusika Kweli.”

Jolvin aliamua kumvuta mkono make hata kumsikiliza hamsikilizi yupo busy kuangalia mbele.

   “” Ndo unakuwaga busy kiasi hiki!? Unapenda furaha Sana? ” Kuna kitu nataka nikuulize, Kwanini ulidanganya kuwa waumwa? hukutaka niende kwa Anelisa?”

   “” Mhuu! Aa aa.. naumwa tumbo, kichwa! Halafu kumbe hukutaka nipone!?”

   “” Swali…. Kwanini hutaki niwe karibu na Anelisa!? Kuna shida Mimi nikiwa nae?”

Gori alikuna kichwa Kwanza huku akiangalia upenyo wa kutoka pale, ikiwezekana aelekee bathroom!”

   “” Unataka kunikimbia? Wewe nakujua vizuri! Najua ulipanga na Bibi! Sawa’ najua Bibi huwa hampendi Anelisa ndio, ndio hadi kwenye ugonjwa? Kwaajili yako nimezima simu ili Anelisa asinipate sijui hata ananifikilia Nini mtoto wa watu huko aliko!?  ” Kama unafikili nikienda kwa Anelisa ni sababu nampenda Mimi sipo hivyoo!?”

“” Aaah! Kwani ni ugonvi Kaka White! Ishatokea bhana! Wewe tafuta njia nyingine na sio kunilalamikia hapa!”

“” Ee… Unasemaje make unang’ona chinichini!?”

Gorii alijua kubananishwa mpaka alihisi joto mwili mzima, aliwaza Kama ataendelea kumjibu ile tabia ya kuzira inaenda kutokea muda huo. Aliamua kufunga macho Kwanza baada ya kuona mawenge huenda Kofi linaenda kutua usoni, alishikilia shavu zake kwa mikono miwili Kisha alisema;-

“” I’m sorry.. Kaka White! Yote nimefanya ni kwasababu simwamini Anelisa huyu ni muongo kwako atakusababishia matatizo! Wewe niamini Mimi na usiende kumwambia mama kwa hiki kilichotokea! Mama ataanza kunichukia Mimi!”

Ile anakuja kufungua macho anakuta kiti kipo wazi lakini Simu ya Jolvin ilikuwa pale! Aliangaza huku na kule hamuoni mtu alichukua Simu ya Jolvin akawa anaikagua kila sehemu huku akiibonyeza! Kwa bahati mbaya aliiwasha, alianza kutetemeka huku akitizama sehemu ya kuizima kabla hajakutwa.

Message za Anelisa zilianza kumiminika, alianza kuzisomea kwa juu wakati zinaingia.

   “” Jovii.. sikutegemea Kama ungenifanyia hivi leo?  Mimi naumwa, kukwambia uniletee dawa ndio kosa langu?” 

  “” Jovii… Au unaniogopa baada ya kukwambia nakupenda! Unahisi ukija huku nitalazimisha unipatie majibu?”

  “” Jovii… Au ni kwasababu ya huyo Binti wa kijijini! Ulivyompeleka nyumbani kwao Kuna kitu kiliendelea?”

   “” Jovii… Siku yenyewe kabla sijakwambia nakupenda.. ndio ulitaka kuniambia unae mtu unae mpenda Kama si Gorii ni Nani huyo!?”

“” Kweli naumia Sana Jovii..  kwa ulichonifanyia huenda ni makosa yangu kukwambia ukweli wangu, au ulitaka niendelee kukuficha Hadi lini!? Ni kitu ambacho siwezi kukivumilia, naumia Jovii…

Gorii alimaliza kusoma Kisha alishusha pumzi ndefu, baadae alicheka Kwanza.

   “” Huuu! Joviii… Naumia sana, au kwakuwa nimekwambia nakupenda ndio waniogopa? Jovii.. Daah! Anelisa huyu ana mambo yaani anajua kulalamika huyu! Kidogo tu Jovii…. Mhuu! Kupatwa kwa Kaka White, sa’ sijui ni ya kweli? Anyway watajuana wao.

Muda huo Jolvin ndio anafika pale alimkuta Gorii kaiweka Simu Kisha yupo busy na kitochi chake akicheza Game huku akicheka mwenyewe kana kwamba anafurahia sana. 

Jolvin alimtizama Kisha akaangalia Simu yake imegeuzia kwa nyuma, alimtizama tena Gorii Kisha alishika simu yake ile anaigeuza anabonyeza aishike vizuri anakutana na mwanga.

“” Sheat!! Ndio Wewe umefanya hivi!? Gorii niseme kipi unielewe!? Nimezima kwaajili ya Anelisa, ona Sasa anapiga Simu hapa, shika umpokee!”

“” Kaka White! Mtoto wa Mishoki family” “unatizamwa hapo!?”

Jolvin ndio anageuka upande wa pili ndio anaona watu wote wamemtolea macho, ilibidi awe mpole alikaa huku akiendelea kusoma message za Anelisa.

   “” Sherehe imemalizika, Twende nyumbani!”

   “” Mbona badoo!!?”

   “” Weee!! Unaenda huendi!!?”

   “” Basi twende!!”

Baada ya kufika kwenye Gari, Gorii aliogopa kukaa mbele alikaa nyuma, Jolvin aliishia kumtizama baada ya kuona kafunga mlango aliondosha gari kwa speed Kali hadi walipofika nyumbani, alishuka kwenye gari Kisha alimshika mkono Gorii hadi chumbani Kwake akafunga Mlango.

   “” Unajifanya kuogopa!? Wakati kwenye hiki chumba Ushawahi kuingia kabla! Ilikuwa ni masaa tu Mimi kufika ukaingia humu, halafu leo hii waogopa kukaa humu! Leo utalala humu.

   “” Hapana! Hapana… Kaka White! I’m sorry! Naomba uniache niende sio tabia nzuri kukaa chumba Cha mkaka! Nitamwambia Bibi pia akuombe msamaha tulidaganya!”

   “” Mhuu! Leo unaogopa kukaa kwenye chumba Cha wanaume! Siku ile chumbani kwa Rich ulifata nini! Au mnae Mahusiano hadi uingie!”

Gorii alishidwa kujibu ilibidi aanze kulia, alikumbuka siku yenyewe Jolvin amkalie kifua wazi, mara amwangukie hapo akajua ameisha.

Jolvin alibaki kumtizama Kisha alivuta kiti akakaa mbele yake.

   “” Nijibu maswali yangu Kwanza ndio uondoke! Nataka uniambie ukweli!! Je, ulisoma message za Anelisa!?”

Gorii alifanya kukataa! Jolvin alifanya kurock mlango Kisha funguo akaweka mfukoni, Alimrudia Tena Gorii.

   “” Namjua Gorii huwa ni mkweli! Yeye hadanganyi! Narudia tenaa… Ulisoma message!? Kwanini uliiwasha Simu!?”

   “” Aaa… aa.. Niliwasha kwa bahati mbaya baada ya kuona umeondoka pasina kuaga ndio nikachukua Simu yako, kwa bahati nzuri Message zikaanza kuingia kwa juu nikawa nasoma ila sio zote!?”

   “” Unajua kuongea ukweli ee! Baada ya kusoma ukachukua maamuzi ganii!?”

  “” Nikaigeuza Simu! Nikaiweka mezani!  naomba unisamehe tu.. ila Anelisa anajua kulalamika yule..'”

Jolvin aliamua kurudisha Kwanza kiti sehemu yake! Kisha alichukua funguo akafungua mlango.

   “” Ayaa simama kwanza!”

   “” Ahsante Kaka White… kwa kutonipiga! Niliogopa sana.””

   “” Rudi hapa… Umeona ulivyosimama umepaachaje? Basi tandika kwanza.

  “” Nimemaliza Mjukuu wa Bibi… Siku ile ulisema nisikuite Kaka White! Leo nimetengua kauli.

Jolvin alibaki kumtizama asiseme chochote, alifungua mlango akaushikilia huku akimwachia atoke.

Ile kutoka Gorii alikimbilia Chumbani Kwake akajitupia kitandani akifanya kugalagala kwanza, Ghafra mlango uligongwa alikuwa ni Jolvin.

“” Kaka aa. W.. sorry! Mjukuu wa Bibi’ si yameisha tenaa! bado unanifuata tu?”

Jolvin alifanya kumpatia simu yake muda ule aliisahau kitandani.

   “” Thank you!”

Usiku Bibi alifika kutoka kazini alikuwa amechoka Sana! Jolvin baada ya kumuona Bibi kafika alimletea kinywaji kwanza atumie huku akimpa pole na majukumu.

Gorii muda huo alikuwa akichungulia akiangalia Jolvin atamwambia Nini Bibi! Kila akichungulia aliona wanaongelea maada za biashara! Baada ya kuona hamna dhari alitembea kwa kunyata akaingia jikoni kusaidiana na wapishi! 

Mama nae muda huo alifika, alimuita Goryanah amletee Maji ya kunywa.

Huku kwenye hifadhi ya vyakula Gorii alikuwa tayari kabebelea maji kutoka kwenye frigi alianza kuzunguka muda wote akiwaza jinsi atavyo peleka maji sebuleni, aliweka jagi kwanza Kisha alikimbia kuchungulia ajue Jolvin kakalia upande upi ili amfikie Mama.

Wakati anachungulia Jolvin alikuwa katoka! Alirudi haraka akachukua jagi Kisha akamletea Mama sebuleni, alimimina kwenye Glass baada ya mama kumaliza kunywa alimuuliza..

   “” Vipi khari? Jolvin kaniambia unaumwa kichwa kwasasa unajisikiaje!?”

Gorii alishituka kwanza kabla hajatoa jibu. “” Aaah huyu si kaniambia najiuguza imekuwaje tena amwambie naumwa?”

Wakati anataka kujibu Jolvin alifika huku kabebelea Dawa.

   “” Mama nimemletea dawa zake! Atakuwa anatumia kutwa mara tatu!?”

Gorii pamoja na Bibi walitoa macho kutizama dawa huku kila mtu akijiuliza. “” Mbona ni dawa nyingi?”

   “” Aa lakini Mjukuu wa Bibi’ Mimi naendelea vizuri! Nitachukua baadhi tu, hizo zingine kaa nazo nikiugua nitakuwa naja kuchukua!”

   “” Wewe si unaumwa!! Au ulidanganya ndio maana hutaki dawa! Mtu nimejitoa kumuita Doctor! Akashauri nikuchukulie dawa halafu unakataa!?”

  “” Basi Jolvin.. atakunywa tu hebu leta hizo dawa! Ni zipi anakunywa sahii!?”

Mama aliongea huku akimshika mkono Gorii, akae karibu yake! Jolvin alichukua Kama aina nne za dawa akampatia, Mama ilibidi amuulize…

  “” Mbona ni dawa nyingi  Jolvin!?”

   “” Doctor ndio kasema!!” 

Jolvin alijibu.

Gorii alichukua maamuzi magumu, alikunywa dawa zote huku akibaki kumtizama Jolvin ambae haoneshi kujali kabisa! Kwa Bibi muda huo aliamua kufunga macho asione kinachoendelea. Baada ya kumaliza kunywa aliomba akapumzike chumbani, mama akawa amemruhusu.

Baada ya kumaliza kula kila mtu aliingia chumbani akabakia Jolvin akisoma sebuleni, Bibi kila muda alikuwa akichungulia Kama Jolvin kalala akimbie chumbani kwa Gorii’ kumtizama. Jolvin alilijua hilo akawa amebakia pale makusudi.

   “” Bibi haulali leo!? Naona muda wote unanichungulia? Wewe kalale Gorii” anaendelea vizuri nipo namlinda hapa!”

Bibi alirudi huku akiwa na aibu kafumwa.

  “” Mjukuu nae anamlinda wakati yupo sebuleni, Gorii huko chumbani sijui anaendeleaje?”

Jolvin baada ya kumaliza kusoma alichukua chupa ya maziwa aliyokuwa nayo pale Kisha alielekea chumbani kwa Gorii, Aligonga mlango… Gorii ndio anasimama kuja kufungua.

   “” Bibi sijafa bhana! Ila Mjukuu wako Kuna siku ataniua hivi hivi naona!!”

Ile anafungua mlango anashangaa kumuona Jolvin. Jolvin nae aliishia kucheka Kisha alimjibu.

“” Kwa tabia yako hiyo na utakufa kweli!”

Alimpatia maziwa anywe!  huku akikaa kumtizama jinsi anavyoyanywa.

   “” Kumbe unagopa kufa? Mimi nikajua muda ule waekit kuumwa ulitaka ufe Kweli! ” Naona Hujakataa maziwa?”

  “” Na Wewe hupendi nife pia! Usingeleta maziwa..’ Mimi nisingekunywa” kuleta kwako unaonesha hutaki nife!”

   “” Na siku nyingine urudie hayo maigizo! Muite Bibi aingie ndani naona kakaa mlangoni Kama mlinzi!”

Gorii ndio anafungua mlango alimuona Bibi akikimbia kuishilia chumbani Kwake ilibidi acheke tu huku akirudishia mlango.

   “” Kaka White! Nashukuru!! Pia nisamehe!

Jolvin alimwangalia, mtu anaeshukuru na anaeomba msamaha kampea mgongo!

   “” Gorii mtoto mwenye heshima, anae nidhamu, anaheshimu watu wadogo kwa wakubwa! Hii kuongea amekupea mgongo tuiweke upande ganii!?”

Gorii alimgeukia alikumbuka Yale maneno aliwahi kuyaongea Jolvin, siku wakutane kwenye chumba Cha Rich na leo kayarudia japo kayabadilisha kidogo, ilibidi amuulize;?

   “” Kaka White…. Huwa ninakukosea Sana mpaka uanze kunielezea tabia kupitia mafumbo pale ninapokuuzi!?”

Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya Goryanah Kumtumia Chochote

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM 

Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii editor@kijiweni.co.tz  

20 Comments

  1. Hapa palikuwa pa🔥🔥🔥🔥

    “” Bibi haulali leo!? Naona muda wote unanichungulia? Wewe kalale Gorii” anaendelea vizuri nipo namlinda hapa!”

    Bibi alirudi huku akiwa na aibu kafumwa.

Leave A Reply


Exit mobile version