Ilipoishia ” Muda huo Mama Rich alifika pale alitaka kumkumbatia Gorii amuage, lakini Gorii alimgeuzia mgongo hii ikamuumiza Sana! Alijua tayari chuki aliyoisababisha mwanae Sasa imehamia familia nzima kwaaajili ya mtu mmoja leo furaha haipo tenaa!

Gorii siyo haipendi ile familia ila aliamua aisahau kabisa! Alihisi ni kwasababu ya umaskini wake ndio chanzo hata hawamuani Tena, Alimtizama jinsi mama Rich akiwa anarudi ndani kwa unyonge ilimpelekea hata yeye azidi kulia. 

Endelea 

SEHEMU YA KUMI NA SABA 

Baadae walifika nyumbani! Gori alikalibishwa tena kwenye chumba chake akawa amepaki begi zake! Siku hiyo ilikuwa ni siku ya huzuni kwake hata kula hakula alikuwa akimkumbuka mamake! Mama Doreen alijitahidi kumbembeleza Lakini wapi! Mwisho kabisa alimuacha akae pekee huenda Kuna mambo anataka afanye mwenyewe!

Huku nyumbani kwenye familia ya Mishoki kulikuwa hakukaliki Bibi nae alikataa kula akimhitaji Gorii! Jolvin ilibidi amfuate aongee nae Lakini Bibi alimgomea! Aliamua kumtafuta mamake aongee nae ndipo anamkuta Chumbani akiwa ameshikilia picha ya mmewe pamoja na picha ya Naina.

Alibaki amesimama akimtazama mamake Kisha alisogea karibu na mamake akawa amekaa.

“” Mamaa kipi umekumbuka leo? Sio kawaida yako kuangalia picha ya Baba pamoja na Naina! Wametangulia mbele za haki mamaa!”

“” Namkumbuka binti yangu Naina! Sahii angekuwa umri wa Gorii! Ile haikuwa siku yao ila ni ajali ya kusababishwa tu ndio iliwatanguliza.”

Mama alishikilia picha ile kwa uchungu huku akiwa analia! Jolvin alimkumbatia mamake huku akivuta taswira ya kipindi kile ajari ilivyotokea.

Ilikuwa ni siku moja Babake alitoka kutembea akiwa na Naina muda huo Naina alikuwa na miaka kumi na mbili! Ilikuwa ni siku ya birthday yake Baba aliamua amtembeze sehemu mbalimbali yenye vivutio vitakavyomfanya siku yake iwe vizuri! Baada ya kumaliza kuzunguka majira ya jioni wakiwa njiani wanarudi ghafra lilitokea roli kubwa mbele yake, alijitahidi kulikwepa Lakini kwa bahati mbaya gari yao iliangukia kwenye daraja! Ile wanakuja kuokolewa tayari walikuwa wamepoteza maisha papo!

Kumbukumbu ya Jolvin iliishia hapo! Na kwa muda huo ilikua imepita kama miaka tisa tangu wapoteze maisha! 

Bibi nae huko ndani kulikuwa hakukaliki alikuja Chumbani kwa mwanae ndipo anawakuta wapo kwenye simanzi nzito! Ilibidi na yeye aliunge pale wakaanza kulia wote!

Jolvin aliona ile khari inazidi kumuumiza ilibidi atoke! Aliingia Chumbani Kisha akampigia Esau simu waongee! Alimwelezea kilichotokea lakini ushauri wa Esau alimwambia hii yote ni kwasababu Gorii hayupo! Na hii imewapelekea kuwaza vitu vya nyuma ili kurudisha khari ya awali ni kumrudisha Goryanah!

Esau alikata simu huku akimkumbuka Kweli Gorii, aliamua kumpigia lakini namba yake haipatikani! Ilibidi awajulishe wenzake kile kinachoendelea nyumbani ikiwezekana Kama watampata Gorii wamsihi arudi nyumbani.

Ilipita miezi kadhaa Gori alikuwa amezoea mazingira mapya! Muda huo alikuwa akiishi Hostel! Ule utundu utundu wake ulipungua kidogo huenda ni vile anakua! 

Siku hiyo ilikuwa ni weekend baada ya kutoka Chuoni, aliamua kuja kusalimia nyumbani. Baada ya kufika aliingia Chumbani kwake siku hiyo aliikumbuka simu yake aliiwasha angalau atizame watu waliomtafuta! Ile kawasha tu alikutana na message nyingi kutoka kwa watoto wa Mishoki! Aliamua kuzipuuzia lengo lake lilikuwa ni kutafuta ujumbe wa mamake kama kapatikana! baada ya kuona hamna ilibidi azime simu tenaa! Huku akiendelea kusoma.

Alifungua kitabu chake kwa bahati nzuri au mbaya alikutana na picha aliyopiga na Bibi pamoja na Jolvin siku ile wanazindua duka! Ilimsononesha kiasi fulani make Alianza kuikumbuka ile familia! Alikumbuka jinsi Bibi yake walivyokuwa wakitaniana, baadae kabisa alimtizama Jolvin alikumbuka mambo mengi wamewahi kufanya tangu wakutane nyumbani hata ile siku kampeleka kwao! Pia ile siku walienda kufanya tangazo alimwachia pesa ndefu ambayo imekarabati nyumba yao kijijini.

Mwisho kabisa furaha yake inakatishwa baada ya kukumbuka maneno aliyomtolea siku yenyewe aondoke kwenye familia yao hii ilimuuma Sana!

Wakati akiendelea! Kukumbuka Doreen alifika pale akiwa na ile simu kubwa alimletea Gorii.

   “” Gorii! Leo nimeingia What’s up kupitia namba yako! Ile nimefungua tu Rich kapiga yaani kakukumbuka balaa!

“” Umenikosea bhana! Sikutaka niwe hewani!”

“” Tatizo Wewe huelewi! Si umeshakuwa maarufu! Nimekufungulia page Instagram nikaweka ile picha ulikowa ukifanya matangazo! Hutaamini watu wengi wamekufollow wanataka ukawafanyie matangazo Tena! Hapo utakuwa ukikusanya pesa pasina kutarajia! Kwani hutaki kumalizia Nyumba yenu kijijini!?”

Gorii baada ya kusikia Nyumba tena ilibidi wakae vizuri huku wakianza kuzijibu zile message zilizotumwa na wadau! Kuna mtu alimpigia Gorii kwenye namba ake akimuomba leo jioni aonane nae, muda mrefu Kweli amekuwa akimtafuta hata alipotumia ile namba ya Jolvin aliambiwa yupo busy na masomo ilibidi awe mpole.

Baada ya kukata simu walibaki wakitazamana na Doreen huku akimuomba aende! Watatafuta namna ya kumtoroka mama tenaa!”

Majira ya jioni walijiandaa haraka Kisha wakatoka kimya kimya kuelekea kwenye Hoteli ilipo! Baada ya kufika walimuulizia mhusika! Mhudumu aliomba mlegwa ndio aingie! Gorii alimkabizi begi Doreen huku akimuomba amsubili pale.

Baada ya kufika hutaamini watu wengi walianza kumshobokea Gorii! Huku wakimuuliza habari za alikokuwa make wengi waliamini yupo shuleni na huku karudi likizo!

Gorii Alibaki kuwakubalia huku akiingia kwenye chumba maarumu akawa ameandaliwa vizuri! Ndio akarudishwa kwenye stage afanye shoo kidogo ya kucheza Kisha ndio picha zichukuliwe! 

Kwaujumla zoezi lake lilifanikiwa alipatiwa pesa yake nzuri Kisha alirudi kwa mwenzake.

   “” Gorii umekosea wambie wakuwekee picha kwenye simu! Tuweke kwenye akaunti tuendelee kupata wateja!

   “” Nitamuomba boss! Si akaunti yake tunayo! Atashea lile tangazo nami atanitag huku!”

“” Ooh! Sawa! Kumbe huwa unaakili Sana.

Walifika sehemu ya kuchukua usafiri! Lakini siku hiyo usafiri ulikuwa wa shida Kila daradara itakayopita imejaza! Mwisho kabisa waliona gari private inafika pale! Doreen alifanya kuisimamisha! Ile imesimama tu waliingia kwa haraka haraka.

“” Kaka Masaki.. tuache!”

“” Afadhari tumepata usafiri! Nilikuwa nawaza Kama tutachelewa tutamwambia vipi mama!”

Gorii aliongea huku akiangalia kile kitita Cha pesa Alibaki akizishika shika tu kwa furaha.

“” Nishukuru Mimi! Laah hivyo usingezipata!”

Walicheka kwa pamoja huku wakifurahi! Zile sauti zao zilimfanya Dreva aliyekuwa akiwaendesha alitoa earphones masikioni Kama vile sauti aliifahamu, lakini alijua ni wenge tu! Alionekana ana mawazo Sana kila akipiga hatua anakumbuka maneno ya ndugu zake.

   “” Mrudishe Gorii! Familia haina furaha! Hata biashara ya Duka haiendi tena! Wateja wote wamemkimbia Bibi wanamtaka Gorii!””

“” Wewe Kaka tumefika! Tuache bhana! Mbona husikii.

Gori na Doreen walikuwa wakisaidiana kumuita make alikuwa hawasikii kaweka Earphones. Gorii akaona asimchezee alianza kutafuta upenyo hadi akamfikia dreva Kisha akamtoa ile prouva yenye kofia Kisha akashika usukani akisimamisha pembeni! 

Baada ya kusimamisha ndio anageuka amfokee vizuri! Kabla hajafungua mdomo alibaki amestaajabu baada ya kukutana  uso kwa uso na Jolvin!

Jolvin pia alipigwa na butwaa huku akipepesa macho yake huenda ni Kama vile haamini! Aliishia kumuita Gorii huku akimshika uso! Ahakikishe Kama ni yeye!

Gorii ndio hakili inakaa vizuri alipepesa macho Kwanza kutoa wenge alilokuwa nalo Kisha akaushika mkono wa Jolvin akaushusha chini.

“” Leo ni siku mbaya kwangu! Na hii ni baada ya kukutana nawewe!”

Alitoa pesa Kama elfu kumi akamkabithi Kisha aligeuka afungue mlango ashuke! Doreen alikuwa bado haelewi kinachoendelea alifungua mlango akashuka ili asogee upande wa Dreva aangalie kinachotokea.

   “” Khaaah!! Kaka Jov!!? Ni wewe tena!? Mbona hauji hata nyumbani kutusalimia! Au ni kwasababu ulimfukuza Gorii!”

Doreen alikuwa Kama anatonesha kidonda kwa Gorii na Jolvin! Ilibidi Jolvin amfungulie Kwanza mlango! Wakawa wameshuka wote!

Gorii hakutaka hata kumsikiliza Jolvin alimshika mkono Doreen waondoke lakini Jolvin alimshika mkono Doreen kumzuia wasiondoke!

“” Kaka White!! Unataka nikujazie watu! Naomba mwachie Doreen! Pia sitaki upite njia yangu tenaa!” 

Jolvin aliamua kumuachia kwani kimbembe Cha Gorii anakijua vizuri! Alibaki kuwatizama mpaka wanaishilia Kisha alipanda kwenye gari huku akijiinamia kwenye usukani! Akijilaumu sana yote yaliyotokea ni makosa yake!”

Hata alipofika Nyumbani alikuwa na Mawazo Sana alipitiliza Chumbani kwake! Ile anafika alimkuta Anelisa kamsubili alifika akakaa kwanza Kisha alichukua grass ya maji akanywa.

   “” Anelisa!! Leo tualishe ratiba yetu ya kujisomea naona kichwa hakipo vizuri! tufanye kesho!”

   “” Kwanini Jolvin!? ” Mbona siku hizi umebadilika Sana! Kila tukipanga ratiba unaialisha Nini shida lakini!?”

   “” Ane… Wewe si unawazazi wote! Mimi Sina Baba!”

Jolvin aliongea kwa ufupi lakini hakumanisha vile Kama angesema ni sababu ya Gorii angemkosea Anelisa. Anelisa alimsikitikia Sana Alisimama akamkumbatia kwa muda mrefu Kisha alimkisi kwenye paji la uso huku akichukua Mkoba wake aondoke.

   “” I’m sorry Jov!! Sipendi nikuone unakosa furaha! Natumia muda mwingi kukufanya uwe na furaha sijui nakosea wapi tu! Kama ndo familia wanakulaumu umemuondoa Gorii basi mrududishe uziepuke hizi stress!”

Jolvin alijisikia vizuri! maneno ya Anelisa yalimfariji alitabasamu huku akiongea mwenyewe” ” ukifanya hivyo tutakuwa pamoja na wewe wala hakutaharibika kitu”  alimuita kwanza.

   “” Anelisa! Ni wait..!”

Anelisa alibaki amesimama huku akifikilia kweli Jolvin! Ameshamkazia kabisa japo siku za karibuni Jolvin alimwambia awe rafiki ziku moyo wake ukianza kufumguka kwake atamfanya mchumba na ndio makubaliano yao! Mpaka Anelisa kurudisha mazoea kati yake na Jolvin.

Jolvin baada ya kumfikia alifanya kumkumbatia! Kisha alimtengenezea nywele zake huku akiongea nae.

   “” Kama Gorii ndie furaha ya hii familia! Basi nitamrudisha ili nibaki na amani tu!”

Anelisa alimkumbatia pia! Japo alikuwa na maumivu baada ya kugundua Jolvin ashaanza kumpenda Gorii na Kama atarudi Nyumbani ndio atamkosa kabisa! Hakuwa na jinsi zaidi ya kumsapoti tu.

Waliagana pale kwa furaha huku kila mtu akiendelea na kazi zake! Jolvin akiwa Chumbani kwake siku hiyo alitoa picha zote za Anelisa na Gorii walizopiga hivi karibuni, alichukua picha ya Gorii na Anelisa akaanza kuzipambanisha!

   “” Tofauti ya Anelisa na Gorii, Gorii anae nywele ndefu za kisomari! Pua yake midomo yake! Ni mizuri! “” Anelisa ni mrefu anashep ana mtazamo mzuri na yeye ana macho mazuri! Ila midomo yake sio Kama ya Gorii, mguu wa kawaida… Gorii yeye wa bia! Kuhusu vidole ni vilaini vipo vizuri kwa massage! Gorii vimekomaa sijui kwasababu ya kazi!! Kwenye kupika Anelisa hajui.. Gorii anaweza! Kwenye tabia Anelisa ni mnyenyekevu! Anajua kuomba msamaha! Gorii ndio anawaza kupambana ikiwezekana hata kukudhalilisha anaweza.. lakini ni mtu jasiri anapambana halafu anapedwa na familia hii karibia wote, pia huko mtaani ndio usiseme!! Sijui ni Nini kinanikuta mpaka naanza kumfikilia yeye Anyway nitamrudisha Nyumbani! Kwa Anelisa anaonekana ananipenda kweli sijui nimkubalie hata hivyo familia yake ina uwezo mkubwa.

Huku Nyumbani kwa Gorii siku iliyofuata alirudi chuo akiwa na simu yake kubwa! Muda wote ilikuwa ni kusikilizia apate dili la kutoa matangazo apate pesa ndio yalianza maisha yake rasmi! 

Wakati ametulia hosteli aliijiwa na Madam Kuna watu wanahitaji kumuona! Ile anaenda kuwatizama Alishangaa kumuona Bibi akiwa na Anelisa na ndio wageni wake.

Alifurahi Sana kukutana na Bibi! Siku hiyo walimletea zawadi mbalimbali pamoja na vyakula! walikaa wawili na Bibi waongee! Anelisa aliwapisha.

“” Gorii uje Nyumbani Mjukuu wangu! Kazi zimekuwa ngumu wateja wamenikimbia wote wanataka urudi! Natamani kulifunga duka lakini nashidwa kwasababu Lile duka lilifunguliwa kwaajili yako! Na pesa muda wote tunaziweka kwenye akaunti yako! Uwe unakuja mara moja moja kupaangalia angalau upachangamshe tu!”

Bibi alijitahidi kumuomba mpaka Gorii akahisi huruma! Alimwahidi Bibi kila weekend atakuwa akimtembelea dukani! Lakini sio kuuza.

Walifikia mwafaka lakini baadae Gorii alimuuliza.

   “” Bibi hivi ni Wewe ndie umeambatana na Anelisa? Au tayari ameshakuwa mkamwana katika familia?”

Bibi alitabasamu tu Kisha akamshika masikio.

“” Muda ule nawaza kuja huku alikuwepo Nyumbani! Akaomba anilete, Jolvin yeye kaamua kulizindua upya duka hebu ona crip aliyotupia kwenye page yake!”

Gori alishika simu akaitazama kwa makini, mpaka ikamkosesha furaha!

   “” Mishoki desginer group kwasasa tumewaletea nguo mpya zitakazowapendesha na Sikukuu pia yule Binti yetu mumiliki atakuwepo kuanzia tarehe ishirini na ndie atakuwa msimamizi hapa! Kwahiyo karibuni Sana Sana ukutane na Gorii Goryanah! Anawasalimia Sana huko aliko pia ana hamu ya kukutana na nyie!

Gorii baada ya kumaliza kutizama ile video alimrudishia Bibi simu Kisha alimuuliza.

   “” Kwanini mnadanganya!?”

  “” Hatudanganyi inatakiwa Wewe uwepo ili kufufua lile Duka! Jolvin hakuwa na njia nyingine ya kufanya hivyo! Kajitahidi kukutafuta muda mwingi ili aongee na Wewe lakini uliomba kwa mkuu wa chuo hutaki kuonana na mtu yeyote akutembelee na Kama utataka kitu ulisema utaenda Nyumbani, Jolvin amekuwa akija hapa mara kwa mara angalau akuone lakini imeshindikana! Siku ile ndio alibahatika kukuona kwenye Gari hata alipotaka kuongea na wewe hukumpa nafasi! Alikuja kunihadithia yote haya! Mwisho kabisa akaahidi kusimamia duka lako haijalishi utarudi lini! Anataka awekeze zaidi kwenye account yako kwa kulikuza duka lako!?”

Bibi aliweka kituo, Gorii hadi machozi yalianza kumlenga ndio akamuuliza.

“” Mama yeye yuko wapi!?’

“” Tangu uondoke Nyumbani Mama kwasasa khari yake sio nzuri! Muda wote anamkumbuka Naina pamoja na Babako aliyetangulia mbele za haki siku moja na Naina! Na leo ameenda kuomboleza makabulini huko Nyumbani kwao na Babako!”

“” Naina… Kwani Bibi ilitokea Nini make huwa namsikia Naina tu!?

Bibi alianza kumsimulia jinsi ilivyotokea Hadi wakapoteza maisha! Baadae alimalizia kumwambia.

“” Yote hayo yatokee! Mama Doreen huwa ni rafiki mkubwa na mamako! Alijua mama anapitia wakati mgumu hata alipokupata Wewe toka kituoni alimshilikisha Mamako akakuomba ukae Nyumbani akufanye kama binti yake! Maana hana watoto wa kike! Ujio wako hapa ndani ilikuwa ni furaha mno hasa zile tabia ulizonazo mmefanana kweli na Naina ndo maana familia nzima ilikupenda!”

Gorii Alibaki kulia tu! Mwisho kabisa Anelisa alifika make muda ulikuwa umeisha alimwomba Bibi waondoke huku akimuaga Gorii na kumtakia masomo mema, wao wakaondoka.

Siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya kwake! Hata mood wa kujisomea hakuwa nao aliamua akakae nje pekee kutafakari maneno ya Bibi pamoja na ile familia walivyomuonesha upendo, alichukua simu yake akatizama namba ya Mama Rich akaona isiwe mbaya Kama ndie mama anamkubali acha amjulie khari.

Alipiga Kama mara tatu simu haipokelewi, mwisho kabisa alikata simu akaendelea kukaa pale muda mrefu!

Baadae simu iliita tena ilikuwa ni namba ngeni ilimwelekeza kesho Asubuhi afike kituoni Kuna mtu anahitaji kumuona!”

   “” Atakuwa ni Mama kajisalimisha kituoni ee!?”

Aliongea vile baada ya simu kukatwa! Kisha aliingia ndani kulala.

Usiku huo huo kwenye simu ya Jolvin kuliingia message ikimuarifu afike kituoni Asubuhi.

Asubuhi kulipokucha kila mtu aliwahi kituoni! Gorii alikuwa wa kwanza kabisa kufika kituoni! Japo kulikuwa Kuna watu wengi wamejazana Kuna wafugwa walikuwa wakiletwa kituoni huku ndugu zao walifika kuwaona.

Wakati ule Jolvin alikuwa kashikilia simu yake huku akijiuliza ni kipi kaitiwa pale!? Na yeye aliwaza huenda ni mama Gorii kapatikana! 

Gorii alikuwa akipenyeza mbele za watu ili atizame vizuri mbele, na Jolvin nae alikuwa akifanya vilevile atokeze mbele! Mwisho kabisa Gari la wafugwa lilipita likielekea kituoni! Watu walianza kusukumana huku kila mtu akitaka aone ndugu yake ikawa ni vurugu! Police ilibidi wasogee pale kuimalisha usalama waliripua bomu la machozi baridi ndio usalama ukaonekana.

Lakini Gorii” alikimbilia bombani kunawa Kisha alirudi huku akiita Maama kwa sauti ya juu! 

Bahati nzuri katika wafugwa wale Mama Gorii alikuwepo! Alisikia ile sauti ikimuita! Siku zote unaambiwa Damu ni nzito kuliko maji, mama Alisimama na kuangaza kuangaza huku na kule! Baadae ndio anamuona Gorii akija mbio akikimbilia Lile Gari! Aliangalia nyuma kulikuwa Kuna gari linakuja full.. Gorii nae hakuangalia nyuma yeye alikuwa akimtizama Mama muda wote!

Watu wote walipiga kelele huku wakifunga macho! Wasiamini tukio linaloenda kutokea! Ilisikika sauti ya break lakini kwa pembeni kuliruka damu Hadi kwenye gari! Kisha ukimia ukafata Kama dakika kumi kila mtu akiwa ametulia huku kainamisha kichwa chini haaamini kilichotokea.

Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya 18

Unapomaliza Kusoma Acha Na Comment Yako 

Ulipitwa na SIMULIZI NYINGINE? 

SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya Goryanah Kumtumia Chochote

Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOM 

Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii editor@kijiweni.co.tz  

35 Comments

  1. Henderson Didas on

    😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭 imekuja kuwa jau

  2. Tafadhali Admin tunataka mwisho mwema naona na Mimi mood itaharibika, usifanye nachokiwaza mwandishi 😰😰, Niko chini ya vidole vyako, sitasubuthu kusoma Tena story huku

  3. Admin promis me kwamba aliegongwa sio goryanah wala jolvin stim ya story itaniishaaa mim😪😪😪😪

  4. Godwin Clemence on

    Kama Gory au Jolvin ndo atakuwa kagongwa Mimi nitaacha kusoma story, Kwa sababu nitakuwa nimeumia Sana,😭 lakini kama wakibakia ad mwisho wa story nitatafuta zawadi Kwa ajili ya admin na mwandishi ikiwezekana

Leave A Reply


Exit mobile version