Shirika la Soka nchini Uingereza, FA, limeamua kutomshitaki Luis Diaz, licha ya kukiuka kanuni za ujumbe kwenye jezi alipofunga bao dhidi ya Luton.

Diaz alitoka benchi na kufunga bao la kusawazisha dakika za majeruhi kwa kikosi cha Liverpool walipokuwa wanacheza dhidi ya Luton katika ligi kuu ya Uingereza siku ya Jumapili.

Ilikuwa mechi yake ya kwanza kucheza tangu wazazi wake walipotekwa nyara na kikundi cha waasi nchini Colombia siku tisa zilizopita.

Mama yake alipatikana haraka, lakini baba yake bado hajapatikana, huku waasi wa ELN wakiitisha “dhamana za usalama” kwa ajili ya kumwachilia huru.

Baada ya kufunga bao lake huko Kenilworth Road, Diaz alinua jezi yake ili kuonyesha ujumbe uliosema ‘Libertad Para Papa’ (‘Uhuru kwa Baba’).

Kwa mujibu wa kanuni za FA, wachezaji wanapaswa kujizuia “kuvaa au kuonyesha kitu chochote kinachoonyesha ujumbe wa kibinafsi.” Kawaida, hili lingemfanya Diaz akabiliane na mashtaka kutoka kwa shirika hilo.

Hata hivyo, kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail, viongozi wa FA wameamua kutomshitaki kutokana na mazingira ya kipekee na ukweli kwamba mchezaji huyo wa Liverpool hakuondoa kabisa jezi yake.

Mbali na kuonyesha ujumbe huo chini ya jezi yake, Diaz aliomba hadharani baba yake aachiliwe huru.

Aliandika taarifa kwenye mitandao ya kijamii, akiwasihi kikundi cha waasi kutimiza ahadi yao ya kumwachilia baba yake.

Hapa si mchezaji anayezungumza Leo ni Lucho Díaz, mwana wa Luís Manuel Díaz Mane, baba yangu, mtu mwenye bidii, nguzo ya familia… sasa ametekwa nyara naomba ELN waachilie baba yangu haraka iwezekanavyo,” alisema.

“Pia naomba mashirikisho ya kimataifa kufanya kazi kuhakikisha uhuru wake, Kila sekunde, kila dakika tunahangaika zaidi Hatuna maneno ya kuelezea hisia mbaya za familia yetu, na itabaki hivyo hadi atakaporudi nyumbani.

“Naomba mumwachilie baba yangu sasa hivi, kuheshimu utu wake nataka kushukuru Wacolombia wote na jamii ya kimataifa kwa msaada wenu, Bao hili ni kwa ajili ya uhuru wa baba yangu na watekwa wote nchini mwangu Asanteni kwa msaada wenu.

Kikundi cha waasi cha ELN, chenye msimamo wa Kikomunisti-Kileninisti kali, kimekiri kutekeleza utekaji nyara.

Lakini wametaka “dhamana za usalama” kwenye taarifa mpya waliyotoa kujibu bao la Diaz na ombi lake la umma.

“Tarehe 2 Novemba, tuliiarifu nchi uamuzi wa kumwachilia Bw. Luis Manuel Díaz, baba wa mchezaji Luis Díaz Tangu tarehe hiyo, tumeanza mchakato wa kutekeleza hili haraka iwezekanavyo Tunafanya juhudi za kuepuka matatizo na vikosi vya serikali,” ilisema taarifa hiyo.

Eneo bado lina askari, wanafanya doria, kupeleka wanajeshi, kutoa matangazo na kutoa zawadi kama sehemu ya operesheni kubwa ya kutafuta. Hali hii haiiruhusu utekelezaji wa mpango wa kumwachilia huru haraka na kwa usalama, ambapo Bw. Luis Manuel Díaz hako hatarini.

Ikiwa operesheni zitaendelea katika eneo hilo, zitachelewesha kumwachilia huru na kuongeza hatari.

“Tunaelewa huzuni ya familia ya Díaz Marulanda, ambayo tunawaambia kwamba tutatimiza ahadi yetu ya kumwachilia huru bila masharti, mara tu tutakapopata dhamana za usalama kwa utekelezaji wa operesheni ya kumwachilia huru.

Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa

Leave A Reply


Exit mobile version