Chelsea itamteua Frank Lampard kuwa mkurugenzi mkuu wa muda hadi mwisho wa msimu siku.

Lampard anatarajiwa kuendesha mazoezi siku ya leo

Alhamisi na kuwa kwenye kibarua chake cha kwanza wakati Chelsea itakapopambana na Wolves siku ya Jumamosi baada ya kukubaliana kurudi kwenye klabu yake ya zamani.

Hakuna chochote kilichojadiliwa kuhusu Lampard kubaki zaidi ya majira ya joto, na mchakato wa kutambua na kumteua kocha kamili wa kudumu unaendelea.

Lampard alikuwa Stamford Bridge Jumanne usiku kushuhudia sare ya bila kufungana kati ya Chelsea na Liverpool, saa 48 baada ya Graham Potter kuachishwa kazi.

Lampard, mwenye rekodi ya ufungaji wa magoli bora zaidi Chelsea, alifutwa kazi kama kocha mkuu mwezi Januari 2021. Kisha akachukua nafasi hiyo Everton lakini akapoteza kazi yake mwezi Januari baada ya kudumu kwa chini ya mwaka kwenye jukumu hilo.

Hatua ya kuwa mkurugenzi wa muda kwa Lampard inakuja baada ya Chelsea kufanya mazungumzo huko London na Luis Enrique, aliyekuwa Kocha wa Barcelona na Hispania, juu ya nafasi yao ya ukufunzi.

Enrique mwenye umri wa miaka 52, ambaye hana kazi baada ya kuondoka kwenye nafasi ya kocha wa Hispania baada ya Kombe la Dunia, alishinda taji la LaLiga, Copa del Rey, na Ligi ya Mabingwa na Barcelona mnamo msimu wa 2014/15.

Leave A Reply


Exit mobile version