Barcelona Tayari Kusikiliza Ofa Zenye Kuanzia €70 Milioni kwa Mshambuliaji Mwenye Umri wa Miaka 26

Barcelona itaanza kuondoa wachezaji wengi sana katika dirisha hili la usajili kwa lengo la kupisha usajili mpya katika timu yao.

Ingawa kipaumbele chao kilikuwa ni kumrejesha Lionel Messi Camp Nou, inaonekana kuwa operesheni hiyo imefeli kwani Margentina huyo anatarajiwa kujiunga na Inter Miami kama mchezaji huru.

Baada ya kushindwa kumrejesha Messi, Wa-Katalunya wataelekeza nguvu zao kwa malengo mengine muhimu.

Kwa kawaida, Barcelona itakuwa inatafuta kuwasajili mabeki wa kati, na uhamisho wa Inigo Martinez umekaribia kukamilika, mchezaji mpya wa upande wa kushoto, mshambuliaji wa akiba, kiungo wa kati, na kiungo wa ulinzi baada ya Sergio Busquets kuondoka.

Ili kuhakikisha wanaimarisha nafasi zote msimu huu wa kiangazi, Barça huenda ikalazimika kufanya maamuzi magumu katika soko la usajili, kama kuuza baadhi ya wachezaji ambao wangependelea kuwabakisha. Mmoja wao anaweza kuwa Raphinha.

Kulingana na ripoti ya Tiempo de Juego, Barcelona wapo tayari kusikiliza ofa zinazoanza kutoka €70 milioni kwa Mbrazili huyo. Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu ya England vinaonyesha nia ya kumsajili.

Ripoti za awali zilidai kuwa Newcastle United tayari walikuwa wametuma ofa ya €80 milioni kwa Raphinha, ambayo inafanyiwa utafiti na Barcelona. Ingawa wanaelekea kukubali ofa hiyo kutokana na hali yao mbaya kifedha, mchezaji huyo bado hajako tayari kuondoka katika klabu.

Xavi naye amedai kuwa mchezaji huyo hapatikani kwa uhamisho kwake. Hata hivyo, uamuzi wa mwisho huenda ukafanywa na klabu.

“Raphinha HAPATIKANI kwenye soko. Atabaki Barcelona na atatusaidia sana. Yeye ni mchezaji muhimu sana kwangu, mchezaji ambaye ana umuhimu mkubwa. Yeye anafanya tofauti,” Xavi alisema.

Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa hapa 

Leave A Reply


Exit mobile version